Z
|
itto Zuberi Kabwe,Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia
chama cha ACT -Wazalendo, amewasilisha fikra zake kwa njia ya mtandao wa
kijamii,juu ya mabadiliko madogo yaliyofanywa katika Baraza la Mawaziri.
Katika maoni yake juu ya Baraza jipya la Mawaziri lililofanyiwa
mabadiliko jana, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe
Magufuli,Zitto ametumia fursa hiyo kutoa pongezi na ushauri.
Kwenye
ukurasa wake wa Facebook Zitto Kabwe ameandika ujumbe akiwapongeza
Mawaziri hao walioteuliwa ambao wengi wao ni vijana, huku akiwataka
kuchapa kazi kwa bidii.
“Uteuzi
wa vijana kushika nafasi za juu ni hatua nzuri, naona vijana wengi
wamepewa majukumu makubwa, ninawaombea watekeleze majukumu kwa weledi
mkubwa”, ameandika Zitto Kabwe.
Jana
Rais Magufuli amefanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri na kuongeza
wizara mpya mbili, baada ya kuzivunja baadhi ya wizara ambazo zilikuwa
na vitengo vingi.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI