Thursday, October 5, 2017

MGEJA;KUJIUZURU MAWAZIRI WABADHIRIFU HAKUTOSHI…

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO





M
WENYEKITI wa Taasisi ya Tanzania Mzalendo Foundation,Khamis Mgeja,amepongeza jitihada za Rais  ,John Pombe Magufuli,kupambana
dhidi ya ubadhirifu wa Rasilimali za nchi,na kudai vitendo hivyo ni matokeo   ya Mfumo  ndani ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi.




Mfumo umesababisha baadhi ya Watumishi Serikalini,kutenda ubadhirifu huo, huku akidai utaratibu unaotumika kuwawajibisha hauna tija kwa Watanzania.

Kauli hiyo aliitoa jana mjini Kahama,akiwa mapumzikoni nyumbani kwake mtaa wa Nyasubi Mjini Kahama,alipotembelewa na kuongea na baadhi ya wazee maarufu  wa itikadi na kada mbalimbali za Kisiasa,ambao waliongozwa na Mzee Jozia Kazi Ngwanateleza kutoka Kata ya Malunga,wilayani Kahama.

Wazee hao walitaka kujua hali ya sasa ya nchi inavyoendelea kisiasa,kiuchumi pamoja na masuala ya demokrasia yanayofanywa na serikali ya awamu ya Tano,na kusimamiwa na Rais John Pombe Magufuli.

Mgeja akizungumza na Wazee hao aliwaambia wakati umefika ni vizuri kufanya tathimini ya kina kwa kazi zinazofanywa na Serikali ya CCM awamu ya tano kwa ujumla ikisimamiwa na Rais John Pombe Magufuli,inaonesha dhamira ya dhati kutaka rasilimali za Taifa zinufaishe umma.

Katika mazungumzo hayo Mgeja alisema pamoja na Rais Magufuli,amekuwa akisema mara kwa mara kuwa nchi hii imeibiwa sana, hasa katika maeneo ya Bandari,Makinikia ya Dhahabu,Almasi,Tanzanite,mishahara hewa na wafanyakazi hewa,alidai hayo ni matunda yanayotokana na mfumo mbovu uliopo na kusimamiwa na Serikali ya CCM.


Alisema pamoja na kwamba kila tatizo la wizi na upotevu wa mali za umma linapotokea imekuwa kasumba ya Mawaziri kujiuzuru jambo ambalo Watanzania hawanufaiki nalo hata kwa kijiko cha sukari,kwa kujiuzuru kwao,hivyo hatua zaidi zilipaswa kufanyika ili kuleta tija kwa Taifa.

“ Ni vyema Watanzania wakati umefika tuambizane ukweli,kinachosababisha mianya ya wizi na ubadhirifu wa rasilimali za nchi,ni mfumo uliojengwa ukatungiwa sheria,ukasimamiwa na Watawala wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi za awamu zote zilizopita za pili,tatu na nne na iliyopo sasa ya awamu ya tano,”alisema Mgeja.

Aliendelea kusema kitendo cha Mawaziri wa Wizara husika kujiuzuru mara kwa mara ni sawa sawa na kuwatoa kafara na kudai haingii akilini na haiwezekani Waziri kuamua jambo bila Baraza la Mawaziri ama Rais kujua.

Alisema Nchi nyingi Duniani zimepata anguko la Kiutawala kutoka Chama kilichopo madarakani ambacho kimepewa dhamana ya kuongoza nchi na kulinda rasilimali na kupelekea kupata kashfa nzito juu ya wizi na ubadhirifu wa rasilimali za nchi.

Kwa upande wao Wazee hao,walishauri kama nchi hapa tulipofika tusitafute mchawi wala kuendelea kuchimbua makaburi,hakuna atakayebaki salama tatizo kubwa la nchi yetu iliyopelekea kuibiwa ni sababu ya mfumo ulioasisiwa na Serikali ya CCM.

Wazee hao walimuomba Rais Magufuli,masuala mawili muhimu kwa manufaa ya Taifa,ambayo ni Suala la kukamilisha Mchakato wa Katiba mpya,pili aelekeze kuangalia ubadhirifu katika maeneo mengine haswa masuala ya gesi,maliasili na upande wa miundo mbinu ambapo kuna barabara nyingi zimejengwa chini ya kiwango na tayari zimegharimu mabilioni ya Shilingi.

Walisisitiza juu ya upatikanaji wa katiba mpya kwakuwa itakuwa muongozo mkubwa na muarobaini katika kutekeleza demokrasia,masuala ya kiuchumi na siasa.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI