Thursday, November 2, 2017

LEMBELI,MGEJA WAITESA CCM SHINYANGA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO





M
bunge wa zamani wa Jimbo la Kahama,James Lembeli, na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga,Khamis Mgeja,wamedaiwa kukitesa chama chao hicho cha zamani kwa kwa kuhusishwa
na kupanga safu za uongozi katika chaguzi za ndani za chama hicho.




Wanasiasa hao ambao kwa sasa ni makada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo “CHADEMA”wanasadikiwa kuhusika kupandikiza wagombea wao katika chaguzi zilizofanyika ngazi ya wila na unaotarajia kufanyika,hivi karibuni wa ngazi ya Mkoa.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti tando hili,umebaini katika chaguzi zilizopita za Jumuiya za CCM,na ule wa Mwenyekiti katika wilaya za Shinyanga,Shinyanga Vijijni,Kishapu na Kahama,majina ya Mgeja na Lembeli yalitawala kwa kuhusishwa baadhi ya wagombea kuhusika nao.

Aidha baadhi ya Wajumbe kadhaa katika mikutano mikuu hiyo,kwa nyakati kadhaa wamedaiwa kuonekana wakibadirishana fikra na viongozi hao maeneo mbalimbali wilayani Kahama,hatua inayowafanya baadhi ya Wana CCM kuingiwa na hofu kubwa mkoa wa Shinyanga na wilaya zake,kupata viongozi watakaoongoza chama hicho huku wakiwa mapandikizi ya Mgeja na Lembeli.

Wanadai baadhi ya Wagombea na Wajumbe kuonekana kuwa na ukaribu na wanasiasa hao,ambao wanawatafsiri si wenzao tena tangu walipokihasi CCM Oktoba 2015,na kuhamia CHADEMA,ni sehemu ya usaliti mkubwa unaofanyika katika kipindi hiki cha chaguzi za chama.

“Angalia ushahidi huu wa kimazingira,tangu Mgeja atusaliti na Lowasa kwenda CHADEMA,maisha yake yamekuwa Dar Es Salaam,lakini tangu kinyang’anyiro cha chaguzi zetu kuanza ametia kambi,wilayani Kahama,” Kilidai chanzo chetu ambacho hakikupenda jina lake lianikwe hadharani.

Anasema,“Watu hawa ambao ndani ya CCM walikuwa mahasimu,lakini wakiwa Chadema ni maswahiba wakubwa, wanashirikiana kutupangia safu ili 2020,watupige maana mara kadhaa wameonekana katika maeneo tofauti na makada wa CCM ambao ni wajumbe wa Mikutano Mikuu ya wilaya na Mkoa.”

Hata hivyo akiongea kwa simu,Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga,Haula Kachwamba,alisema japo hawatambui watu hao lakini kutokana na uelimishaji walioufanya kwa wajumbe wa mikutano mikuu ngazi ya wilaya,anaimani wasaliti hao hawakupenya.

“ Unajua kazi ipo kwa wapiga kura,Mimi kura yangu ni moja,wanatakiwa wamuweke nani na hauwezi kujua kwakuwa ni siri,lakini sidhani kuwepo mapandikizi kutokana na uelimishaji tuliokwisha kuufanya,”alisema Kachwamba.

Kwa upande wake Mgeja,alikana kujihusisha na kampeni za kusimika viongozi wa CCM ngazi za wilaya,ama katika uchaguzi unaotarajia kufanyika hivi karibuni wa ngazi ya Mkoa,bali yupo Kahama kwa ajili ya mapumziko na maandalizi ya msimu wa kilimo.

“ Unajua nipo nyumbani kwa mapumziko na ninakutana na Watanzania wenzangu wa dini na itikadi tofauti,kubadilishana fikra kutokana na changamoto za kimaisha zilizopo kwa sasa,sipo kwa ajili ya chaguzi za CCM na watambue mimi kisiasa ngazi yangu ni Taifa si Mikoa ama wilaya,”alisema Mgeja.

Nae Kada maarufu wa CCM Mkoa wa Shinyanga,Paschal Ntare,alisema mitazamo ya Wana CCM wenzake, juu ya miongoni mwao kuwa karibu na mashabiki ama wafuasi wa upinzani kama ilivyo kwa Mgeja na Lembeli,ni uchanga wa kisiasa,kwakuwa si kila wakati watazungumzia siasa bali kuna maisha nje ya siasa.

“Tuache unafiki kinapofika kipindi cha uchaguzi kuchaguliana marafiki,mimi kada wa CCM,sitatengana na Lembeli sababu ni ndugu yangu,wala sintomuepuka Mgeja sababu ya Itikadi,”alisema Ntare.

Aidha;James Lembeli,alidai Busara na Hekima kwa kipindi hiki kwa Wana CCM imetoweka,kutokana na kuanza kupandikiza utengano kwa Watanzania kwa kigezo cha Itikadi ya Vyama,pasipo kutambua Watanzania waliishatoka katika mfumo wa chama kimoja na wanahitaji mshikamano ili kujiletea maendeleo ndani ya Vyama vingi.

“..wanachokiasisi wasije kugeuza ubao kwamba kinaletwa na upinzani maana wao ni mabingwa wa propaganda,lakini watambue wanamuasi Baba wa Taifa,ambae mwaka 1995,aliishi na mwanae Makongoro akiwa Mbunge toka upinzani,”alisema Lembeli.


Katika chaguzi ngazi ya wilaya zilizopita,kampeni za CCM na jumuiya zake zilitawaliwa na majina ya Lembeli na Mgeja yaliyotumika kuwadhoofisha baadhi ya wagombea ambao ni makada wa muda mrefu walionekana na nguvu za kisiasa ndani ya chama hicho,kuwaengua ama kutochaguliwa huku wachache wakishinda kwa mbinde kwa madai ya kuwa karibu na Mgeja na Lembeli.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI