K
|
atika kuhakikisha Maendeleo endelevu
yanapatikana kwa jamii inayoishi pembezoni mwa miji
nchini,asasi ya kiraia ya
HUHESO Foundation, imehamasisha elimu ya utunzaji fedha.
Elimu hiyo ambayo imetimiza miaka
mitatu,imeambatana na kuwezesha uundwaji
vikundi 909 vya kuweka na kukopa wilayani Kahama.
Akiongea katika Kikao cha Bodi ya
Wakurugenzi wa Shirika hilo,kilichofanyika jana Kahama mjini,Mkurugenzi
Mtendaji wa Huheso Foundation,Juma Mwesigwa,alisema upatikanaji vikundi hivyo
ni zao la miradi miwili wanayoitekeleza.
Mwesigwa alisema lengo la kufundisha
elimu hiyo na kuhamasisha kuanzisha vikundi vya kuweka na kukopa ni kuwezesha
wananchi kutambua na kujua namna bora ya utunzaji fedha kwa jamii zilizo mbali
na upatikanaji w huduma za kibenki kwa wakati.
Alisema vikundi 699 vimeanzishwa
kupitia Mradi wa Pesa kwa Wote ( PKW ),unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la
Care Tanzania,ambao wanautekeleza katika Halmashauri tatu zilizo wilaya ya
Kahama za;Msalala na Ushetu sambamba na Halmashauri ya Kahama Mjini.
“Mradi huu unaoisha Desemba mwaka
huu,ulikuwa wa miaka mitatu,lengo ni kuwafikia wanawake asilimia sabini na
thelathini ya wanaume,na hadi katika robo inayoisha Juni 2017,tumefanikisha
kuunda vikundi 51,”alisema Mwesigwa.
Aidha alifafanua vikundi vingine 210 vimetokana
na Mradi wa Sauti,wanaoutekeleza kwa kushirikiana na Shirika la
JHPIEGO katika Halmashauri ya Ushetu,unaofanya kazi ya kuhudumia Makundi
maalumu yaliyo katika hatari zaidi ya kupata maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi wa Shirika la HUHESO Foundation,Shija Felician,alisema jitihada za
shirika lake katika kutoa elimu na kuhamasisha uundaji vikundi unasaidia
kupatikana kwa maendeleo stahiki.
Aliomba Serikali kuthamini mchango huo
mdogo unaofanywa na Huheso kwakuwa unarejesha nidhamu ya fedha katika jamii, na
kuisaidia kukabiliana na mabadiliko ya kiuchumi yanalolikabili Taifa
kipindi hiki.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI