Friday, October 13, 2017

ELIMU,AJIRA BINAFSI KUFANIKISHA TANZANIA YENYE VIWANDA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




W
azazI na Walezi,wameombwa kuwapatia elimu ya kutosha vijana wao huku wakiwashauri kusoma
masomo,yatakayosaidia kujipatia ajira binafsi.




Imebainishwa ajira binafsi itakuwa kichocheo kwa jamii kushikamana na kushirikiana katika Nyanja ya uchumi,hatua itakayosaidia kufanikisha mikakati ya serikali ya awamu ya tano ya kujenga Tanzania yenye viwanda.

Ushauri huo ulitolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Rocken Hill Academy inayomiliki Shule ya Sekondari ya Anderlek Ridges,Alexander Kazimil,katika mahafali ya 9 ya shule hiyo,kwa kuikumbusha jamii kusimamia vijana wao kupata elimu ya kutosha itakayokuwa msaada wa kupata maendeleo.

Kazimil alisema jitihada za serikali kufikia uchumi wa kati kwa kuwa na viwanda,zitakwama pindi vijana wakikosa elimu ya kukabiliana na changamoto za sayansi na teknolojia,kwakuwa Tanzania ya viwanda itajengwa na Watanzania vijana,wenye elimu ya kutosha itakayosaidia mabadiliko makubwa ya viwanda.

Kazimil  aliwahakikishia jamii,pindi ikiwa karibu na vijana wao kwa kuwekeza katika elimu,itakayosaidia kukabili mabadiliko ya sayansi na teknologia itakayokwenda na soko la ajira ikiwemo viwandani,sambamba na kujipatia ajira binafsi ambazo zitakuwa vichocheo vya kuanzisha na kumiliki viwanda vidogovidogo.

Alionya wazazi wenye uwezo kifedha kutowekeza katika elimu kwani katika ulimwengu wa sasa pasipo kuwajengea uwezo wa kielimu vijana wao watakuwa wanawatumbu,iza katika lindi la ufukara kwakuwa watashindwa kushindana katika ushindani wa Kibiashara.

Kwa upande wake mgeni rasmi katika Mahafari hayo ya tisa,Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Kahama,Richard Kilenga,aliwakumbusha umuhimu wa wazazi katika kumuongoza mwanafunzi,kuchagua michepuo yenye tija katika suala la ajira ili kuondokana na ombwe la kuwa na elimu kubwa,lakini akiwa katika hangaiko la ajira.

Kilenga alisema kwa kuwa wazazi wameshaona mengi wengine ni watumishi wa serikali wanaelewa kabisa mtoto akisoma mchepuo Fulani ajira zake ni nyingi kuliko kumuacha mtoto akapoteza muda kusoma elimu ambayo atahangaika nayo kutafuta kazi wakati kuna michepuo mingi ambayo akisoma atapata ajira kwa haraka.

Naye Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Anderlek Ridges,Adamu Lui,aliwaasa wazazi kushikamana na walimu kuhakikisha vijana wao wanatimiza ndoto zao kielimu,kwa kusisitiza misingi ya nidhamu na maadili ili kumuepusha kijana kutumbukia katika matendo mabovu.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI