
M
|
vua
kubwa zinazoendelea kunyesha kwa siku tatu mfululizo,katika mkoa wa Dar Es
Salaam,zimeanza kuleta madhara katika miundo mbinu ya
barabara,kwa kubomoa daraja.
Madhara
yaliyosababishwa na mvua hizo zinazoendela kunyesha kuanzia juzi mchana,ni kukatika
kwa daraja la Kiluvya,linalounganisha mkoa wa Pwani na Dar es Salaam.
Kutokana
na daraja hilo kukatika hudumza za usafiri wa magari ya abiria, mizigo
na binafsi umesitishwa na wananchi wameombwa kutumia barabara ya
Bagamoyo.
Daraja
hilo ni kiungo muhimu kati ya jiji la Dar es Salaam pamoja na mikoa
mbalimbali ya Kaskazini, Kati, Kanda ya Ziwa, Nyanda za juu Magharibu.

Aidha,
mvua hizo zimesababisha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam
yamejaa maji zikiwamo nyumba na kusababisha uharibifu wa mali.
Adha
daraja lingine eneo la Mbezi beach jijini Dar es Salaam ‘maarufu la
Jeshi’ kutokea Kawe limejaa maji na inadaiwa magari kadhaa yamezama na
njia imefungwa.