J
|
amii imeombwa kutojichukulia sheria
mikononi kwa kuadhibu kwa vipigo kisha kuwaua,pindi wanapowashuku baadhi ya
binadamu kutenda vitendo vya uharifu.
Imetakiwa kuwafikisha katika vyombo
vya dola ili sheria ishike mkondo wake na si kuchukua jukumu la kuwaua raia
wasio kuwa na hatia,pindi wanapowahisi ni wezi bila kuwa na
uthibitisho wa kutenda kosa hilo,anaandika
Tunu Herman, Mwanza.
Rai hiyo imetolewa jijini hapa na
Ofisa wa Fedha wa Shirika lisilokuwa la kiserikali la Railway Children,Mgewa
Joseph,alitoa rai hiyo mwishoni mwa wiki alipokuwa akizungumza kwenye ibada ya
mazishi ya vijana wanne wa mitaani waliouwawa na wananchi wenye hasira,kwa kudhaniwa
ni wezi.
Alisema tukio hilo la kusikitisha lililotokea
Oktoba 15 huu majira ya saa nne usiku katika eneo la Nyashana manispaa ya
Ilemela, ni la kusikitisha kutokana vitendo vilivyofanywa kutozingatia sheria
za nchi,na kusababisha tukio hilo la mauaji kuacha huzuni na simanzi
kubwa kwao.
Alisema vijana hao waliouwawa walikuwa
wanafanya kazi naye wakiwa chini ya Shirika hilo tangu mwaka 2014 na
kuthibitisha kuwa kipindi cha uhai wao, hawajawahi kukumbukwa na tuhuma za
uhalifu.
Aliwataja vijana hao kuwa ni
Issa Yusufu(21, Paulo Charles(21) na Anord Maige(17) wote wakiwa ni
wakazi wa Kiloleli katika Kata ya Nyamanoro katika Manispaa ya Ilemela mkoani
Mwanza.
Kwa upande wake Meneja mradi wa
kivuko Abdallah Issa ambaye alikuwa anafanya kazi kwa karibu na vijana hao ,
alisema anasikitishwa na jinsi jamii inavyowachukuluia vijana hao
wakidhani ni wahalifu pasipo kutambua kuwa ni vijana wanaojitambua na wana
mipango mizuri ya maisha kwa siku zijazo.
Alitaka jamii ielimishwe juu ya
umuhimu wa kuwepo kwa vijana hao na washiriki kikamilifu kwa kuwalea kwa
maadili na sio kuiachia serikali, wanaharakati na mashirika yasiyo ya
kiserikali.
Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa
Kikundi cha Mkombozi Elias Mwita ambacho kimewapoteza vijana hao kwenye tukio
hilo, aliiomba serikali vijana wa mitaani ni sehemu ya watu katika jamii na
wasibaguliwe kwa mauaji yasiyo na hatia.
" Wanajamii watambue tunawapenda
na sisi tunahitaji kuishi kwa amani kama wanavyoishi wao”alisema.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo,
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema
inadaiwa kuwa vijana hao ni wezi na kufafanua jeshi la
polisi bado linaendelea na uchunguzi ili kubaini kama ni wezi na watu
wengine watakaobanika kujihusisha na mauaji hayo, hatua kali za kisheria
zitachukuliwa dhidi yao.
“Niwaombe wananchi wanapowakuta
wahalifu wasijichukulie sheria mkononi na badala yake watoe taarifa kwenye
vyombo vya dola ili wakamatwe na kufikishwa mahakamani”, alisema.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI