R
|
ais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli,amewatunuku
kamisheni maafisa 422 wa Jeshi.
Kamisheni hizo,amezitunuku kwa Wanajeshi,ambao wamehitimu
mafunzo mbali mbali kwenye chuo cha Jeshi Monduli mkoani Arusha.
Tukio hilo ambalo limefanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha
Mjni, limehudhuriwa na viongozi mbali mabali wa kitaifa na mafisa wa
Jeshi nchini pamoja na wananchi mbali mbali wa mkoa wa Arusha.
Kabla ya kuwatunuku kamisheni maafisa hao wa jeshi, Rais Magufuli
alikagua gwaride maalum, na kutoa zawadi kwa maafisa wa jeshi watano
waliofanya vizuri zaidi kwenye masomo yao.
Tukio hilo la Rais Magufuli kuwapa Kamisheni Maafisa wa Jeshi katika
uwanja wa Sheikh Amri Abeid ni la kwanza kufanyika katika uwanja wa wazi
badala ya viwanja vya jeshi wilayani Monduli.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI