Friday, September 22, 2017

FISI WAZUA HOFU KAHAMA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO






H
OFU imetanda kwa wakazi wa Kijiji cha Kakebe,wilayani Kahama,juu ya kuliwa Fisi,kutokana wanyama hao
kudaiwa kurandaranda nyakati za jioni hadi usiku hata  kuvamia kwa  Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ihashi kijijini hapo,Daudi Martini,  na kula kuku 41 kati ya 60.



Kutokana na tishio la Wanyama hao, serikali ya kijiji hicho imewataka wananchi kuacha mara moja kuchota maji nyakati za usiku  kwa hofu ya kuliwa na fisi,anaandika Salma Kipara.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Daniel Mabula,ametoa agizo hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofika kijijini hapo kwa lengo la kujionea uharibifu uliofanywa na mnyama huyo katika familia ya mwenyekiti wa Kitongoji cha Ihashi.

Mwenyekiti huyo alisema  baada ya fisi kuvamia banda  na kufanikiwa kula kuku 41,walitoa taarifa ngazi mbalimbali zinazohusika wilayani Kahama,huku wakitoa onyo kwa wananchi kutochota maji visimani nyakati za usiku licha ya kuwepo uhaba wa maji safi na salama.

Tabu Katoto shuhuda wa tukio hilo anasema licha ya wananchi kuokoa mifugo mingine  pamoja na maisha ya familia hiyo serikali inapaswa kulichukulia uzito suala hilo kwani wanyama hao wamekuwa wakilandalanda mitaani na kuhatarisha amani.
Naye  shuhuda mwingine wa tukio, Michael Shuiyili, alisema  wanyama hao wanajihifadhi katika pori lililojirani na kijiji,hivyo kuiomba serikali kupitia idara ya wanyama pori ifanye msako,kabla wanyama hao hawajafanya uharibifu mkubwa.

“… kwani huku kunashida ya maji fisi atakula wake zetu wanaoenda kulinda maji usiku,” alisema  Shuiyili.


Naye mwanamke mmoja aliyejitamburisha kwa jina moja  la Veronika  alisema pia mnyama huyo alikula mbwa wake mchana kweupe na alishuhudia pia ngombe mkubwa kwa jirani yake akiliwa na fisi hao.



Kwa upande wake Katibu tawala wa Wilaya ya Kahama, Timoth Ndanya,alikiri kuwepo kwa wanyama hao na kusema kuwa tayari Serikali wilaya imetoa agizo kwa Halmashauri ya Mji wa Kahama,kushughulikia suala hilo  na zoezi la msako juu ya wanyama hao litaanza mara moja kwa kushirikiana na idara ya wanyama pori.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI