S
|
iku chache baada ya
Wanakijiji wa Kakebe,Kata ya Nyandekwa kuingiwa hofu ya kuliwa fisi,aliyevamia
na
kula kuku 41,hali hiyo imejitokeza tena Mjini Kahama,baada ya Fisi mmoja
kuonekana akirandaranda ndani ya eneo la Hospitali ya Wilaya.
Katika tukio
hilo lisilo la kawaida lilisababisha kuibua taharuki kubwa kwa wagonjwa na watu
waliokuwa katika hospitali ya Mji wa Kahama,huku likizidisha Hofu ya wananchi
katika maeneo mbalimbali juu ya kuibuka
kwa Wanyama wa aina hiyo katikati ya Mji,anaandika Salma Kipara.
Akizungumza
na Wandishi wa Hospitalini hapo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kahama,
Dr. Lucas David alisema tukio hilo lilitokea jana,majira ya saa 12 alfajiri kwa Fisi huyo ambaye hakujulikani alipotokea, kufaulu kuingia ndani ya
hospitali hiyo.
Alisema
kuwa licha ya eneo la Hospitali hiyo kuwa na uzio mkubwa,fisi huyo alifaulu
kuingia kupitia upande wa chuo cha
Manesi ambapo kuna tundu linalopitia
karibu na chumba cha kuhifadhia maiti.
Kwa upande
wake Mganga mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dkt. Fredirick Malunde alisema
baada ya kuonekana kwa mnayama huyo walitoa taarifa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri
ya Mji,ambaye naye aliwaarifu watu wa Idara ya Maliasili ambao walifanikiwa
kumuua fisi huyo kwa kumpiga risasi tatu.
“ Hali hii
sasa inatisha mjini kwetu,si kawaida,tumejawa na hofu,tunatafakari usalama wetu
hasa kwa watoto wetu ambao hulazimika asubuhi kwenda Shule,tuna maswaali yasiyo
na mjibu juu ya wanapotoka fisi hao,”alisema mkazi wa Kahama mjini,Aidan
Mwahengera.
Tukio la
fisi huyo linakuja siku moja baada ya taarifa kuwa kundi la Fisi limevamia na
kukatakata mabomba ya maji ya Mradi wa Kilimo cha Mbogamboga wa Kikundi cha
Songambele katika kata ya Nyandekwa Halmashauri ya Mji wa Kahama.
Kabla ya
hapo,katika Kata hiyo iliyo katika Halmashauri ya Mji wa Kahama,Fisi,alivamia nyumbani
kwa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ihashi kijiji cha Kakebe,Daudi
Martini, na kufanikiwa kula kuku 41 kati ya 60.
Hata hivyo Katibu
tawala wa Wilaya ya Kahama, Timoth Ndanya,aliwatoa hofu wakazi wa wilaya ya
Kahama kushambuliwa na wanyama hao kwa kudai tayari Serikali wilaya imetoa
agizo kwa Halmashauri ya Mji wa Kahama,kushughulikia suala hilo na tayari
utekelezaji umeanza kufanywa na Maafisa wa Idara ya wanyama pori.