Friday, September 22, 2017

MKE AFANYA MAUAJI YA KUTISHA,ACHINJA MUMEWE KAMA KUKU!

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




N
i ukatiri na unyama wa hali ya juu,baada ya
  mwanamke wa kabila la Kisukuma,Zena Mohamed (28),kumuua mme wake Bakari Salehe (35); Mzaramo,kwa kumchinja na kisu shingoni upande wa kushoto.


Inaelezwa kuwa wanandoa hao walikuwa wamegombana,ndipo mke akamsubiri mmewe alale ndipo alipoteleza unyama wake huo kwa kumchoma kisu tumboni na shingoni,anaandika Salma Kipara.


Tukio hilo limetokea Septemba 20,2017,saa mbili na nusu usiku katika kitongoji cha Malenge kijiji cha Jomu,Kata ya Tinde,Tarafa ya Itwangi,wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga.


Mashuhuda wa tukio hilo wamesema,“Baada ya kutekeleza tukio hilo,mwanamke huyo alifungua radio kwa sauti ya juu kisha kufunga mlango kwa kufuli na kuondoka kukimbilia kwa mama yake mzazi anaeishi Shinyanga Mjini.

“…..alipofika akamwambia mama kuwa amefanya mauaji,hali iliyomfanya mama atoe taarifa polisi na kufanikisha kukamatwa kwa mtuhumiwa”.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Haule amesema tukio hilo limetokea wakati wanandoa hao walipokuwa wanapigana katika ugomvi uliotokea nyumbani kwao.

“Chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi baada ya mke kupokea simu ya mume wake iliyokuwa ikiita na kisha kusikia sauti ya mwanamke mwingine na kuhisi kuwa ni hawala wa muwe wake,ndipo ugomvi ulipoanzia”,ameeleza Kamanda Haule.

Kamanda huyo wa polisi amesema wanamshikilia mtuhumiwa kwa mahojiano zaidi na ametoa wito kwa wananchi kujiepusha na kuachana na vitendo vya dhana ya wivu wa kufikirika.

“Tuache kufikiri kuwa mwanaume akiongea na mwanamke au mwanamke akiongea na mwanaume kwa njia ya simu au njia ya kawaida lazima kuna mahusiano ya kimapenzi,jambo ambalo siyo kweli hasa kutokana na masuala ya utandawazi katika dunia hii ya leo”,ameeleza Kamanda Haule.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI