Thursday, June 29, 2017

SHILLINGI 40 KWA KILA LITA YA MAFUTA YAWATISHA WAKULIMA WA MPUNGA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO






O
ngezeko la Shilingi 40 katika kila lita moja ya Mafuta ya Taa,Petroli na Dizeli lililofanywa katika Bajeti ya Serikali ya


Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka 2017/2018,imebashiriwa kwa kiwango kikubwa kushusha uzalishaji wa zao la Mpunga.



Katika Bajeti hiyo iliyowasilishwa hivi karibuni na Waziri wa Fedha,Dk.Philip Mpango,ambayo imefuta leseni ya Magari na tozo hiyo kuhamishia katika ongezeko hilo la mafuta,limedaiwa ni mwiba mchungu kwa mkulima wa Tanzania,hususani wa zao la Mpunga,anaandika Shaban Njia.

Afisa Uendelezaji wa masoko kutoka Baraza la Mchele Tanzania Godfrey Rwiza,alibainisha hayo  wakati wa kikao cha wadau wa mnyororo wa thamani wa zao la mpunga kutoka Kanda ya Ziwa,kwa kusema ili mkulima wa mpunga afikie malengo serikali inatakiwa kuliangalia suala la ongezeko la shilling 40 kwa kila lita moja ya mafuta.

Rwiza alisema ongezeko hilo lililofanywa halitamsaidia mkulima wa zao la mpunga katika kuongeza thamani ya zao lake,hasa kwakuwa tayari anawajibika katika kuchangia asilimia 24 katika bajeti ya Serikali,hivyo walistahili kupewa kipaumbele katika kuwasaidia ili wapate kuboresha kilimo chao zaidi na si kuwakandamiza kwa ongezeko hilo la asilimia 40.

Alisema kuelekea uvunaji na utayarishaji wa mashamba kwa msimu ujao wa kilimo,umewaogofya wakulima wengi ambao wamejikuta wakipaki matrekta ya kulimia mashamba,mashine za kuvunia mpunga kwa kuogopa   ongezeko hilo.

Anasema, “..kutokana na hali hiyo haitashangaza,kuona wakulima wakirejea kuanza kutumia mfumo wa uvunaji wa kizamani ambao huwa unaacha mpunga mwingi shambani bila mkulima kutambua,kwakuwa hatamudu kugharama za ununuzi wa mafuta.”

Alisema Tanzania inazalisha mchele kwa asilimia 70, ikiwa ya pili katika ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara,huku  dunia ikitambua mchele mzuri hupatikana  nchini,hivyo serikali ingefanya jitihada za kumsaidia mkulima kusudi aendelee kuzalisha mchele mwingi kwa kuvuna kisasa,pasipo kubakisha mpunga shambani ili Taifa lizidi kunufaika Kimataifa.

Nae Mwakilishi kutoka Jukwaa la Taasisi zisizo za kiserikali zinazofuatilia bajeti ya Tanzania(FORUMCC), Jonathan Sawaye,alishauri serikali kufungua milango ya wafanyabiashara wa mchele kuuza mazao hayo nchi za nje hali ambayo itafanya bei kuwa chini na kumfanya kila Mtanzania kumudu gharama za maisha.

Alisema kuwa hapo awali kilo moja ya mchele ilikuwa ikiuzwa shilling 900 hadi 1100 lakini kwa sasa Watanzania wananunua kilo moja ya mchele shilling 2000 nakuongeza kuwa serikali kuzuia wakulima na wafanyabiashara kuuza mchele nje ni kufanya bei kuongezeka na kuwa ghali kwa Watanzania kumudu maisha.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama Fadhiri Nkurlu ambae alikuwa mgeni rasmi katika warsha hiyo ya wadau wa mnyororo wa thamani wa zao la mpunga kutoka kanda ya ziwa,alisema serikali inatambua uwepo na umuhumu wa wakulima wa zao la mpunga kwa kuchangia asilimia 24 ya bajeti ya nchini.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano ipo bega kwa bega katika shughuli za ukuaji wa kiuchumi hasa katika sekta ya kilimo na kuongeza kuwa wakulima kwa ujumla,wanatakiwa kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki ambacho serikali inafanya tathimini ya wingi wa hali ya chakula na pindi itakapotoa majibu itaweza kuwafungulia masoko na kuuza nchi za nje kama ilivyo ada.

Hata hivyo Nkurlu amewataka wafanyabiashara hao kufungua viwanda vidogo vidogo vya kukoboa mpunga ili kufungua fursa ndogo ndogo za ajira kwa vijana wanaozunguka hovyo mitaani bila kufanya kazi hali ambayo itasaidia kupunguza wimbi la watoto wa mitaani.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI