Tuesday, June 7, 2016

MTENDAJI KATA AWAFUNDA WAKULIMA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



KATIKA kuhakikisha mkulima hapunjwi katika mauzo ya mazao yake,Serikali Kata ya Isaka imepiga marufuku Wafanyabiashara kutoka maeneo mbalimbali nchini kufika eneo hilo wakiwa na vipimo visvyo stahili vinavyomnyanyasa Mkulima.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Isaka,Mwanaidi Mustafa Mzee,katika mikutano ya hadhara iliyoitishwa na Diwani wa Kata hiyo;Gerald Mwanzia,ambapo alisema atahakikisha anawachukulia hatua kali za kisheria Wafanyabiashara watakaofika na kumpunja Mkulima.

Afisa Mtendaji huyo aliwaomba wakulima kutokubali kuendelea kunyanyasika kwa kuendekeza shida zao,bali wahakikishe wanauza ziada ya mazao yao kwa faida kwa kutumia vipimo sahihi vinavykubalika.

“Kwakuwa ni kawaida kutumia vipimo vya asili,kama ndoo za plastiki,basi ni marufuku mfanyabiashara kuja ndoo yake bali wazikute kwenu ambazo mmeridhia kuwa haziwapunji,msikubali kutumia ndoo zao maarufu kwa jina la Msumbiji zinakupunjeni na kumpa faida kubwa zaidi Mfanyabiashara,”alisema Afisa Mtendaji huyo.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Isaka,Mwanzia,alisema Kamati ya Maendeleo ya Kata yake imeanza mkakati wa maendeleo kwa kutafiti changamoto katika sekta za Elimu na Afya,huku wakianzisha mfuko wa kuendeleza sekta hizo.

Mwanzia alisema wanahitaji kuboresha sekta hizo ziwe na tija kwa Kata hiyo hivyo ni budi wananchi washikamane na Kamati ya Maendeleo kwa kuchangia mfuko huo,ambao utaanza kujikita zaidi katika kuboresha miundo mbinu katika sekta za Afya na Elimu.

“Tusihadaike na kufaulu Elimu Bure pasipo kufanya jitihada za kuboresha miundo mbinu yake kama majengo ya madarasa,ambayo bado mwananchi nguvu zake zinahitajika na si kutegemea serikali pekee,”alisema Mwanzia.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI