Wednesday, June 8, 2016

JESHI LA POLISI LASAMBALATISHA MKUTANO WA CHADEMA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




NI TAHARUKI!Iliyoukumba mji wa Kahama kwa masaa manne, Baada Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga jana kuwasambaratisha kwa kutumia mabomu ya Machozi  na gari la maji ya washa wafuasi  na Viongozi wa Juu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliokuwa wakitaka kufanya mkutano wa hadhra kuzindua Opresheni Okoa Demokrasia.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa saba za mchana katika kiwanja cha CDT kilichopo mjini Kahama,wakati viongozi hao wa ngazi za juu wa Chama hicho waliopokuwa wakitaka kufanya mkutano wa kufungua kampeni ya operesheni okoa demokrasi kanda ya ziwa,ndipo askari polisi wa wilayani Kahama waliongezewa nguvu na wenzao kutoka Shinynga walipousambaratisha mkutano huo.
POLISI wakiingia eneo la Mkutano


Katika tukio hilo pia ilishuhudia Viongozi wa Chadema wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe magari yao yakimwagia maji ya kuwasha baada ya kuingia katika Viwanja hivyo vya CDT tayari kwa kuanza Mkutano wao huo,na kulazimika kuondoka ndipo askari kuendelea kutupa mabomu ya machozi na kusababisha kuzua taharuki kwa wananchi wa eneo hilo.

WANANCHI waliokuwa katika Mkutano wakiserebuka kwa kuwazomea Polisi.
Baadhi ya vijana hawakuafikiana na vitendo vya jeshi la polisi hivyo kuanza kuwarushia mawe,jambo lililosababisha miongoni mwao kukamatwa,na askari polisi kuendelea kulitawala eneo hilo hadi mitaa ya jirani kwa kumwaga maji washa na mabomu ya machozi,hatua iliyozidisha taharuki kwa wakazi wa eneo hilo hususani Waislamu ambao walishindwa kuandaa Futari kwa ajili ya kufuturu.

Tukio hilo pia liliathiri biashara mbalimbali zinazofanyika eneo hilo ikiwemo mama Lishe waliamriwa na polisi kuzifunga na kuondoka,vingine wakibaki watajua ni Chadema na watawashughulikia kwani wao wanachoangalia;"Hapa ni kazi tu,kusambaratisha kila kiumbe katika maeneo hayo"

GARI la Polisi likiwa na askari likiingia eneo la Mkutano.
Hata hivyo baada ya kutokea hali hiyo ya sintofahamu katika Viwanja hivyo huku wananchi wakikimbia ovyo kuimbia mabomu ya mchozi yaliyokuwa yakipigwa na Askari wa Jeshi la Polisi kutoka Wilayani Kahama kwa kushirikiana na wale waliopo mjini Shinyanga waliokuja kwa ajili ya kuongeza nguvu ili kusambaratisha mkutano huo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya tukio hilo Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe alisema kuwa kitendo walichofanyiwa na Jeshi la Polisi sio cha kiungwana na kuongeza kuwa taarifa za kufanya Mkutano wao huo walikuwa nazo tangu jana na hiwezekani kuwazuia leo kufanya Mkutano.

GARI za Polisi zikiwa na askari eneo la Mkutano
Mbowe alisema kuwa hawataacha kufanya mikutano yao hiyo kwani haki ya kila Mwananchi kupata taarifa na kuongeza kuwa kwa sasa Wanakaa vikao vya ndani kwa ajili ya kujadili suala hilo na ikibidi watalifikisha Mahakamani kwa fujo walizofanyiwa.

“Kwa sasa hatuwezi kuongea kitu kwa undani zaidi tupo katika vikao vya ndani kwa ajili ya kujadili tukio hilo na ikibidi tutalifikisha katika vyombo vya sheria kwa ajili ya kutolewa maamuzi kwa undani kwani kila c chama kina uwezo kufanya mikutano ili mradi wafuate sheria” alisema Mbowe.

KATIKA uwanja wa Mkutano wananchi wakizomea polisi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Mika Nyange amethibitisha kutoa kwa tukio hilo na kuongeza kuwa walisitisha Mkutano huo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo zile za kiintelejensia ambazo waliokuwa nazo  kuhusu Mkutano huo kuwa kungetokea machafuko na kulikuwa na makundi yaliyokuwa yamejipanga kufanya vurugu.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI