Tuesday, June 7, 2016

DIWANI ISAKA ASISITIZA MAOMBI YA JPM,KWA VIONGOZI WA DINI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



VIONGOZI wa dini wamesisitizwa kuzidi kuliombea Taifa sambamba na wananchi ili wajenge mioyo ya kizalendo iliyopandikizwa na waasisi wa taifa hili,kwa kujitoa kuchangia shughuli za Maendeleo katika maeneo wanayoishi.

Diwani wa Kata ya Isaka,Gerald Mwanzia,aliyasema hayo katika uzinduzi wa Kwaya ya Mtakatifu Fransisco wa Sale ya Dhehebu la Romani Katoliki,Parokia ya Isaka,ambapo alisema jamii wamekuwa wagumu kuchangia shughuli za maendeleo,hivyo kustahili kuombewa.

Alisema Viongozi wa Dini wanastahili kuunga jitihada za Rais wa Awamu ya tano,John Magufuli,kwa kumuombea aendelee na jitihada alizozianzisha za kutetea maslahi ya umma,sambamba na kuiombea jamii kuwa na moyo wa kizalendo na kujitoa kuchangia maendeleo ya nchi.

“Viongozi wa dini mnawajibu mkubwa kuomba na kuwaongoza waumini wenu kwa kuwajenga katika imani za kizalendo,na hili litekelezeni hata kwa kupitia kuwezesha vikundi vya Kwaya kutoa ujumbe kupitia nyimbo zao,”alisema Mwanzia.

Aliongeza kusema, “…ili Taifa lifanye vyema linahitaji kuombewa,na kwakuwa wananchi nao wagumu kuchangia maendeleo kwa kunung’unika pindi watakiwapo kuchangia shughuli za maendeleo,huku wakitaraji maendeleo ambayo kwa yakini watajiletea wenyewe,nao waombewe.”

Kwa upande wake Paroko wa Kanisa la Isaka,Peter Kadundu,aliasa jamii kuwa na moyo wa upendo,kuvumiliana na kusameheana huku ikizingatia kulijenga Taifa kwa kuzingatia maadili mema.

Akisoma risala,mwanakwaya,Michael Emmanuel,alisema albamu yao hiyo iitwayo,Yatafakari Matendo yako,ni ya kwanza kutoa ikiwa na nyimbo tisa,ambapo mauzo yake wanatarajia kuyatumia kununua kinanda na vifaa kadhaa vya kanisa kwa lengo la kuendeshea Ibada.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI