Tuesday, June 7, 2016

WANAFUNZI NYANG’HWALE BADO WANAKETI CHINI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


PICHA ya Maktaba.

IMEELEZWA pamoja na mkakati wa Serikali,kuhakikisha ifikapo Juni 30 mwaka huu, wanafunzi wote nchini kuketi katika madawati,Shule ya Msingi ya Hussein Nasser iliyopo wilayani Nyang’hwale,mkoani Geita,tatizo bado ni kubwa,kufuatia robo tatu ya wanafunzi wake,kuendelea kuketi chini.


Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo,Godfrey Malandi,alisema hayo wakati wa makabidhiano ya madarasa manne yaliyojengwa na Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu,uliopo wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga,ambapo alisema tatizo la madawati shuleni hapo ni kubwa na jitihada za kumaliza tatizo hilo zinasuasua.


Mwalimu Malandi alisema Shule hiyo ina wanafunzi 439,huku ikiwa na madawati 97,ambapo miongoni mwake yakiwa yamekarabatiwa na kukiwa na upungufu wa madawati 120,hali inayofanya wanafunzi zaidi ya nusu kuendelea kuketi chini.

Alisema sambamba na changamoto hiyo shule yake inakabiliwa pia na ukosefu wa vyumba vitatu vya madarasa huku walimu wakiishi eneo la mbali na shule kutokana na kutokuwa na nyumba za walimu za kutosha.

“…tunakabiliwa na upungufu wa nyumba tano za walimu,pia ukosefu wa huduma ya maji safi na salama hatua inayosababisha wanafunzi kutembea umbali mrefu kupata huduma hiyo.”Alisema Mwalimu Malandi.

Aidha Kaimu Meneja wa Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu,unaomilikiwa na Kampuni ya madini ya ACACIA,Benedict Busunzu,alisema kutokana na kufahamu changamoto za kielimu,umekabidhi miradi miwili yenye thamani ya Shilingi Milioni 550.kwa serikali ya wilaya ya Nyang’hwale.

Busunzu alisema uongozi wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu,umetekeleza miradi hiyo kupitia Mfuko wa ACACIA Maendeleo,wakiwa na imani itachangia juhudi za utoaji wa elimu bora kwa wanafunzi.

Ameitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa madarasa manne ,katika shule hiyo iliyopo kijiji cha Mwasabuka katika Kata ya Mwingilo,ambapo darasa moja likijengwa kwa asilimia mia moja na mgodi,mengine mawili kwa nguvu za wananchi na mgodi huku moja wakilifanyia ukarabati.

Aliendelea kusema sambamba na hayo pia Mgodi umetekeleza mradi wa ujenzi wa nyumba moja ya mwalimu,yenye uwezo wa kuchukua familia mbili na matundu 12 ya vyoo.

Kaimu Meneja huyo alikabidhi mradi wa Jengo la kisasa la maabara tatu za Sayansi kwa Masomo ya Fizikia,Kemia na Bailojia katika shule ya Sekondari ya Nyijundu na kuwahakikishia Mgodi kuendelea kuchangia shughuli za maendeleo katika eneo linalozunguka uwekezaji wao.

“Mgodi kujenga miundo mbinu imara kama majengo,ni endelevu ambapo umejiwekea mkakati unaotekelezeka kila mwaka katika kusaidiana na jamii zilizo jirani na Mgodi,kama uwajibikaji wa Mgodi kwa jamii,lengo letu ni kufanikiwa pamoja na jamii.”Alisema Busunzu.

nayozunguka eneo hilo ione faida ya uwepo wa Mgodi,na kubainisha utekelezaji huo hauhusiani na tozo la ushuru wa huduma unaostahili kulipwa katika wilaya hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale,Ibrahimu Marwa,alisema jamii ni vyema ikajenga mahusiano mema kwa kushirikiana na Mgodi kuhakikisha unafanya kazi zake kwa amani ili uzidi kuchangia maendeleo katika wilaya hiyo.

“…ni pongezi za dhati zimfikie Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale,Mheshimiwa Hussein Nasser, kwa jitihada za kufanikisha kuanzishwa kwa shule ya msingi ambayo imeboreshwa na Mgodi,lakini nasi wananchi tuwahakikishie usalama Mgodi katika shughuli zao ili tuzidi kunufaika nao.”Alisema Mkuu wa wilaya.

Alitumia fursa hiyo kudai serikali ya wilaya itahakikisha agizo la serikali la kuhakikisha wanafunzi hawaketi chini ifikapo Julai na kuuomba Mgodi uone umuhimu wa kuhakikisha wilaya ya Nyang’hwale inaondokana na tatizo hilo.

Hivi karibuni Mgodi wa Bulyanhulu umekabidhi Shilingi Milioni Mia Nne(440,000,000/-)kwa taasisi ya Benjamin Mkapa kwa ajili ya mradi wa kuboresha huduma za afya katika Halmashauri ya Msalala,Wilaya ya Kahama,mkoani Shinyanga.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI