Thursday, May 12, 2016

SABA WA FAMILIA MOJA WAUAWA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

WATU saba wa familia moja katika wilaya ya Sengerema,mkoani Mwanza,wameuawa kikatili,kwa kuchinjwa na watu wasiofahamika walipokuwa wamelala nyumbani kwao.
 
Mauaji hayo yalitokea saa nane usiku wa kuamkia jana,katika kijiji cha Sima wilayani humo,huku watu wanne wa familia hiyo wakinusurika kifo.

Taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari wa Mkoa wa Mwanza, Atley Kuni ambaye alifuatana na Mkuu wa Mkoa huo, John Mongella na Kamanda wa Polisi Mkoa, Ahmed Msangi katika eneo la tukio, alisema watuhumiwa katika tukio hilo hawajajulikana.

Kuni aliwataja waliopoteza maisha katika tukio hilo kuwa ni Augenia Philipo (62), Maria Philipo (56), Yohana Mabula (20), Regina Aloyce (12) na Mkiwa Philipo (13) huku wengine wawili wakitambulika kwa jina moja kila mmoja kuwa ni Donald na Samson.

Aidha, chanzo cha mauaji hayo ya kikatili hakijajulikana, ingawa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Zainab Telack alisema huenda mauaji hayo inawezekana yakawa ni ya kulipiza kisasi. 

Vyanzo vingine vinaarifu kuwa mauaji ya namna hiyo ni ya kawaida katika maeneo hayo, hasa msimu huu ambao kaya nyingi zinakaribia msimu wa mavuno.

“Bado kuna mkanganyiko juu ya chanzo cha mauaji hayo, wapo wanaosema kuwa huenda ni ya kulipiza kisasi lakini pia wengine wanasema yanatokana na msimu wa mavuno, lakini tunaamini uchunguzi wa Polisi ndio utakuja na majibu sahihi na ambao umeshaanza kazi hivi tunavyoongea,” alisema Kuni.
 
Baadhi ya majirani wa familia hiyo walidai mauaji hayo yanaweza kuwa yamechochewa na uhasama wa mashamba,huku baadhi yao kutokana na kutokea mauaji hayo wameanza kuzikimbia familia zao,wakihofia kukamatwa kusaidia upelelezi.
 
Hata hivyo walidai tukio la namna hiyo ambalo pia linahusishwa na kisasi,halijawahi kutokea wilayani humo,hivyo baadhi yao kuingiwa na hofu ya kukumbana na mkono wa dola pasipo kuhusika na tukio hilo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI