Thursday, May 12, 2016

KONTENA 115 ZA SUKARI ZAKAMATWA DAR

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

 

 
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam ameamuru vyombo vya dola kuchunguza kontena 115 ya sukari iliyokuwa inasafirishwa kwenda nchini Uganda.

Sukari hiyo ilikuwa imehifadhiwa kwenye Bandari Kavu (ICD) moja iliyopo Barabara ya Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Agizo hilo lilitolewa Dar es Salaam jana baada Makonda akiwa ameongozana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema baada kufanya ukaguzi katika bandari Kavu na baadhi ya maghala ya kuhifadhi nafaka.

Akizungumza jana Makonda alishangazwa kuona kontena hizo 115 ambazo zilikuwa njiani kusafirishwa nchini Uganda.

"Naambiwa sukari hii iko katika makontena 115, lakini vyanzo vyangu mimi vinaonesha kuwa hapa kuna makontena ya sukari 164, lakini sisi tumetembelea ghala hili wametuambia kuwa wana eneo lao la kuwekeza mizigo yao, lakini si huku sasa inakuwaje tena makontena haya yaletwe huku tena... yamechanganywa ili yasionekane sasa naamuru uchunguzi ufanyike mara moja,"alisema Makonda.

Makonda alisema ni lazima Watanzania wajue kuwa kazi hii inapofanyika hakuna kuweka suala la uchama, kwani maendeleo yanahitajika kwa kila mtu aliye ndani ya chama chake.

Alisema ameambiwa sukari hiyo ilikuwa inasafirishwa kupelekwa nchini Uganda, lakini wameamua kubadilisha kibali kwa kuwa nchini kuna tatizo la sukari.

Hata hivyo alisema hakubaliani nalo kabisa kwani huo ndiyo mchezo wa wafanyabiashara kukwepa kodi kwa kuingiza mzigo na kudai kuwa ni wa nje ya nchi, lakini wanautumia ndani ya nchi.

"Hii inatokana na wafanyakazi wasio waaminifu ambao wanashirikiana na wafanyabiashara hao kukwepa kodi kwa madai kuwa mizigo hiyo ni ya nje ya nchi, huku wakiitumia ndani ya nchi," alisema Makonda.

Makonda pia aliamuru kufanyike uchunguzi wa tani zaidi ya 1,700 za sukari za mfanyabiashara huyo ambazo ziliingizwa nchini kwa ajili ya kutumika viwandani.

Katika hatua nyingine Ofisa Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) aliyejulikana kwa jina la Ambrose Bahati, alishindwa kumtajia Makonda siku ambayo kontena hizo zilianza kuingizwa kwenye bandari kavu hiyo licha ya mamlaka hiyo kuwa na ofisi kwenye ICD hiyo.

"Kontena hizi ni nyingi sana hivyo ni ngumu kujua zote ziliingia lini," alisema Ofisa huyo wa TRA. 

Mmoja wa maofisa wa ICD hiyo (jina linahifadhiwa) alisema,sukari hiyo iliagizwa hapo ikiwa inasafirishwa kupelekwa Uganda.

 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI