JAMII
katika Kata za Mwaluguru,Mwakata,Mwanase,Isaka na Jana,katika Halmashauri ya
Msalala wilayani Kahama,wameaswa kutorubunika na tamaa za mpito,kwa kuuza mazao
yao,badala yake wanatakiwa kuhifadhi chakula kinachotosheleza familia zao huku
wakiuuza ziada kwa ajili ya kufanyia shughuli za Kimaendeleo.
Agizo
hilo lilitolewa na Afisa Tarafa wa Isagehe,Mwalimu Reuben Kadigi,kwa Madiwani,Maafisa
Watendaji wa Kata,Vijiji,Viongozi wa Serikali za Vijiji,Vitongoji na vyombo vya
usalama katika Kata hizo,ambapo alisema kumekuwepo tabia ya jamii kutumia
pasipo uangalifu mazao yao,kwa kuuza kisha kufanya anasa.
Mwalimu
Kadigi,alisema Kata hizo hupata zao la mpunga kwa wingi,lakini kutokana
na kutokuwa makini katika suala la uhifadhi,
hususani Wanaume kuuza kwa lengo la kufanya anasa pasipo kuangalia mahitaji katika
familia zao,husababisha kuwa na mahitaji ya chakula toka serikalini.
“Chakula
cha ziada ndicho kiuzwe kwa maslahi ya familia, si kwa lengo lililozoeleka kwa viongozi wa Kaya,pesa kufanyia anasa za ngono,ulevi
uliokithiri pasipo kutambua wanazitumbukiza familia zao katika njaa siku za
usoni,hivyo jitihada zifanyike kudhibiti hali hiyo,”alisema Kadigi.
Kwa
upande wake Diwani wa Kata ya Isaka,Dr.Gerald Mwanzia,alisema ili jamii kuepuka
njaa ni vyema ikapatiwa elimu ya kina katika uhifadhi wa chakula,kwa kutambua
kiwango kinachohitajika katika familia
zao kwa idadi ya watu katika Kaya kwa mwaka mzima.
Afisa
Mtendaji wa Kata ya Mwakata,Haji Omari,alisisitiza elimu kutolewa kwa wanaume
wenye mfume dume ambao hujisahau kipindi hiki kwa kuuza vyakula kwa lengo la
kujitumbukiza katika starehe,huku akitaka sensa ifanyike ili kubaini kila kaya
imepata kiwango gani cha mazao.
Hata
hivyo Afisa Mtendaji wa Kata ya Mwalugulu,Wiliam Kashindye,hakuafikiana na
fikra hizo kwa madai zimechelewa kutokana na baadhi ya jamii kuuza mazao yao
yakiwa shambani kwa baadhi ya wafanyabiashara kwa lengo la kujipatia fedha za
kujikimu.
Nae
Diwani wa Kata ya Mwakata,Ibrahimu Sixberth,alisema suala la uhifadhi chakula
linahitaji usimamizi wa dhati kutoka kwa Maafisa Watendaji wa Vijiji na Kata
kwa kuwajibika kubaini kiwango cha mazao
kila Kaya kusudi itakayobainika kuuza isije
kupatiwa msaada pindi mahitaji hayo yatapotokea.
Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesisitiza kutumia vyema mvua za masika ili
kupata mavuno mengi ya mazao na kutishia kumuajibisha Mkuu wa Mkoa pindi eneo
lake litabainika kuwa na njaa ilhali kulikuwa na mvua za kutosha.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI