Wednesday, April 27, 2016

ALIYEUA KICHAA AKISAKA UTAJIRI KUNYONGWA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



THOMAS Barasa amehukumiwa kunyongwa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kichaa,Samuel Njoroge,ili kutimiza matakwa ya ushirikina kujipatia utajiri.

Hakimu Ngenye Macharia wa Mahakama Kuu ya Eldoret,ya Jijini Nairobi,alitoa hukumu hiyo jana baada ya kuridhika na upande wa mashahidi,baada ya kesi hiyo kuunguruma kwa kipindi cha miaka mitano.

Kulingana na ushahidi ambao uliwasilishwa mahakamani hapo,mshukiwa alitenda unyama huo kwa kushirikiana na watu wengine ambao hawakuwa mahakamani,baada ya kushawishiwa na mganga aliyetajwa kwa jina moja la Omonding wa eneo la Mpakani,atafute viungo vya mwili wa binadamu kwa ahadi ya malipo ya Sh.500,000.

Inadaiwa kuwa Barasa na wenzake walitumia pombe aina ya Chang’aa,kama kivutio cha kumnasa marehemu aliyekuwa na tatizo la akiri.

Ushahidi uliowasilishwa ulionyesha kuwa Barasa kwa kushirikiana na wenzake walimuua na kumkatakata Njoroge baada ya kumlewesha chang’aa,kisha kutupa mwili wake katika shimo ambalo lilikuwa kando ya nyumba ya mshukiwa,Septemba 4,2010.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI