Saturday, April 30, 2016

TUCTA YAHITAJI KIMA CHA CHINI MSHAHARA 750,000/-

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



KESHO Wafanyakazi wote nchini wanaungana na wenzao Duniani,kuadhimisha siku yao,huku Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(TUCTA)likihitaji kima cha chini cha mshahara wa mfanyakazi wa umma kiwe Sh.750,000/-na kisikatwe kodi.

Katibu Mkuu wa TUCTA,Nicholaus Mgaya,amesema Utawala wa awamu ya tano chini ya Dkt.Magufuli,uliwaahidi mabadiliko wafanyakazi,hivyo nao wanahitaji mabadiliko yanayolenga kuboresha maisha yao.

TUCTA imepata kuingia katika mgogoro mkubwa na Serikali ya awamu ya nne chini ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete,walipotishia kugoma wakishinikiza kima cha chini cha mshahara kiwe Sh.315,000/-.

Hata hivyo mgomo huo haukufanikiwa baada ya Kikwete kuweka wazi kuwa Serikali haina uwezo huo na kuwataka wafanyakazi wasikubali ushawishi wa Mgaya,bali akiwaambia akili za kuambiwa wachanganye na zao.

Hadi Awamu ya nne ikimaliza muda wake imeacha kima cha chini cha Mshahara  Sh.240,000/ kwa mfanyakazi wa sekta ya Umma,ambacho anaendelea kulipwa Mtumishi wa kada hiyo.

Mgaya ameitaka Serikali ya Awamu ya Tano,kuongeza nguvu katika kupunguza matatizo mengi yanayowakabili wafanyakazi ikiwemo mishahara midogo isiyoendana na gharama za maisha.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI