Sunday, May 1, 2016

TCRA YATOA ONYO KWA WAUZA SIMU.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania(TCRA),imewaonya  wauzaji wa vifaa vya mawasiliano ya mkononi(simu)kuacha kufanya hila ya kubadilisha namba tambulishi  ya vifaa hivyo(mobile devices)kwa lengo la kupata wateja kipindi hiki cha kuelekea kuzimwa kwa simu bandia.

Onyo hilo lilitolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,Mhandisi James Kilaba,wakati akitoa tathimini  ya hali halisi kuelekea ukomo wa matumizi ya simu bandia nchini,Juni 16,mwaka huu,kwa kubainisha ni kosa kisheria kwa wauzaji wa simu kubadilisha namba hizo.

Mhandisi Kilaba alisema kumekuwepo hila zinazofanywa na wauzaji wa simu,kubadilisha namba tambulishi ambazo kufikia Juni 16,mwaka huu simu hazitafanya kazi,kwa kuweka namba za hadaa kusudi wafaulu kuuza simu hizo,jambo ambalo ni kosa kisheria.

Hivyo alitoa onyo kwa wauzaji watakaobainika kubadilisha namba hizo,watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kulipa faini ya Sh.Milioni 30 au kifungo kisichozidi miaka kumi.

Hata hivyo aliwakumbusha wateja pindi wanaponunua simu wanapaswa kuhakiki ili kubaini kama hazitokuwa na matatizo baada ya mwezi Juni,hasa baada ya kubaini kuwepo kwa vitendo vya hila vinavyofanywa  na wauzaji kwa kuingiza namba mpaya kusudi wafanikiwe kuuza simu zao.

“Wateja wanapaswa kuwa makini kipindi hiki kuelekea Juni 16,mwaka huu,kwani kumekuwepo hila kwa baadhi ya wauzaji simu kuingiza namba mpya kusudi wafanye biashara,lakini watambue hizo ni hila zitakazojenga chuki,kwani muda ukifika hazitafanya kazi,”alisema Mhandisi Kilabo.

Aliwasihi wauzaji hao kuhakikisha wanakuwa waaminifu katika ya biashara ya simu,ikiwa ni pamoja na kuepuka kutoa bei za punguzo za simu za simu huku wakitambua simu hizo ni bandia.

Alisema tangu Desemba mwaka jana hadi kufikia April mwaka huu,TCRA imetoa elimu juu ya kuhakiki simu katika mikoa kumi nchini,huku ikijiandaa kufanya zoezi hilo katika mikoa mingine kumi.

Ameitaja mikoa ambayo wanataraji kutoa elimu hiyo kati ya mwezi Mei na Juni,kuwa ni Kagera,Lindi,Morogoro,Shinyanga,Pwani,Mtwara,Geita,Mara,Simiyu na Mwanza.

Alisema kutokana na uchambuzi wa namba tambulishi (IMEI)uliofanyika Machi mwaka huu imebainika kuwa idadi ya namba tambulishi ambazo hazina viwango zilikuwa asilimia 13 tofauti na Februari mwaka huu ambapo ilikuwa asilimia 18.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI