Saturday, April 30, 2016

JPM AJITOSA KIANA SAKATA LA LUGUMI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



JAPOKUWA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Magufuli,hakuutaja mkataba husika,lakini kitendo cha kulitaka Jeshi la Polisi kujiepusha na kashfa zinazosemwa,ni kana kwamba amejitosa kwenye kashfa za ufisadi unaozungumzwa kufanyika baina ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd.

Rais Dkt.Magufuli akiongea jana mkoani Dodoma kwenye kikao kazi,cha makamanda wa polisi wa mikoa,mawakili wafawidhi wa mikoa na wakuu wa upelelezi wa mikoa na vikosi,alisema mikataba ya ovyo iliyoingiwa imelidhalilisha jeshi hilo,huku akiitaka ofisi ya Mwendesha Mashitaka na Polisi kujirekebisha kwa kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia maslahi ya Taifa.

Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd na Jeshi la Polisi nchini walitiliana saini mwaka 2011 kwa ajili ya kufunga vifaa vya kuhifadhi alama za vidole 108,katika vituo vya polisi na kuzua gumzo kwa kipindi hiki hapa nchini.

Utata wa Mkataba huo umeifanya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali(PAC),kuunda Kamati ndogo ya kufuatilia.
RAIS John Magufuri akiongea na Makamanda wa Polisi wa Mikoa.

Makubaliano ya Mkataba huo yalikuwa ni Kampuni ya Lugumi ifunge vifaa hivyo 108 katika vituo vya Polisi kwa gharama za Shilingi Bilioni 37,lakini mpaka sasa inadaiwa ni vifaa 14 vilivyofungwa huku Kampuni hiyo ikiwa tayari imeishalipwa asilimia 99 ya malipo ambazo ni Sh.Bilioni 34.

Kuna madai utekelezaji wa mkataba huo tata uliozua mijadala kila kona nchini umewahusisha vigogo wa serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani,Charles Kitwanga na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu,Said Mwema,wanaodaiwa kuhusika.



KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI