Wednesday, April 27, 2016

TMA YATABIRI MVUA KUBWA,KUNYESHA UKANDA WA PWANI,VISIWANI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA),imetoa tahadhari katika mikoa ya Ukanda wa Pwani na Visiwani Zanzibar,kwamba mvua kubwa inatarajiwa kunyesha kuanzia April 26 hadi 29,mwaka huu,na kwamba inaweza kusababisha mafuriko.

Taarifa kutoka TMA inaeleza kunyesha kwa mvua kubwa yenye kiwango cha milimita 50 ndani ya saa Ishirini na nne,ambayo itaambatana na upepo mkali unaozidi kasi ya Kilomita 40 kwa saa na mawimbi yasiyozidi mita 2.0.

Taarifa hiyo inabainisha kiwango cha uhakika ni asilimia 80 itakayonyesha katika mikoa ya Tanga,Dar Es Salaam,Mtwara,Pwani,Lindi,Morogoro na Visiwa vya Pemba na Unguja.

Pia mvua hizo zinatarajia kusambaa katika maeneo ya mikoa ya Kilimanjaro na mashariki mwa Manyara.

Taarifa hiyo ilieleza kwamba mvua hiyo inatokana na kuwepo kwa mgandamizo mdogo wa hewa katika pwani ya Tanzania unatokana na kilichokuwa kimbunga aina ya Fantala.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI