Wednesday, April 27, 2016

YANGA KUUSOGELEA UBINGWA LEO,AMA KIPORO KUCHACHA?

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



LIGI Kuu Tanzania Bara(VPL)inaendelea leo kwa kukamilisha michezo miwili ya viporo;Yanga ambao ni Mabingwa watetezi,watakuwa wenyeji wa maafande wa JKT Mgambo,kutoka Kabuku,Handeni Tanga,mchezo utakaochezwa uwanja wa Taifa Jijini Dar Es Salaam huku Azam FC wakiwakalibisha Majimaji ya Songea katika uwanja wao wa Chamanzi.

Yanga watashuka dimbani huku wakiwa na kumbukumbu ya kutoshana ubavu na maafande hao katika mchezo wa raundi ya kwanza,uliochezwa uwanja wa Mkwakani Tanga.

Kocha Msaidizi wa Yanga,Juma Mwambusi,anasema kikosi chake kipo vizuri na wanatarajia watapata matokeo mazuri,huku Kocha wa JKT Mgambo,Joseph Lazaro,akijinasibu kufuata pointi tatu katika mchezo huo.

Katika mchezo utakaopigwa Uwanja wa Chamanzi,Kocha msaidizi wa Azam FC,Dennis Kitambi,amesema wanachohitaji ni ushindi ili waendelee kuwepo katika mbio za Ubingwa wa VPL,huku Kocha wa Majimaji akisema anaamini kutokana na maandalizi walioyafanya wataibuka na ushindi.

Yanga inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 59,mechi 24,ikifuatiwa na watani zake wenye uchu wa Ubingwa baada ya kuukosa kwa kipindi cha miaka mitatu,Simba SC,yenye pointi 57,mechi 25,huku Azam FC ikiwa na pointi 55,mechi 24,hivyo ushindi wa Yanga leo utawasogeza  karibu katika kutwaa taji na kulitetea kwa mwaka wa pili mfululizo.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI