Wednesday, March 2, 2016

WANAKIJIJI WAUKATAA MRADI WA BWAWA LA MAJI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

MWANAKIJIJI Sibitali Nsumba akitoa maelezo kwa Mbunge.


BAADHI ya wananchi katika kijiji cha Isanga,Kata ya Idahina,Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama,wameukataa mradi wa bwawa la maji uliokuwa ukitolewa msaada kutoka nchini Uingereza kupitia Shirika la Oxfam.

Badiliko la kuukata mradi huo ambao awali waliuafiki,lilianza kuwasilishwa na Sibitali Nsumba,alipodai Katika Kikao chao na Mbunge wa Jimbo la Ushetu,Elias Kwandikwa,kuwa pamoja na kwamba alijitolea hekari tano kwenye shamba lake la Mpunga, ili bwawa hilo lichimbwe,lakini ameahirisha.

Nsumba alisema katika kikao chao cha kwanza aliafiki na kuwa ridhaa kutoa eneo lake hilo,lakini baada ya kugundua kulikuwa na udanganyifu wakati wa kupitisha mradi huo,hayuko tayari kutoa kuridhia eneo lake kutumika tena katika mradi huo.

MBUNGE wa Jimbo la Ushetu,Elias Kwandikwa akitoa ushauri.



Alisema wakati wa Kikao cha Kwanza cha kupitisha Mradi huo,utakaogharimu zaidi ya Shilingi Milioni 150,walielezwa kwamba ungeweza kutumia hekari tano tu, lakini baada ya upembuzi yakinifu kufanyika, bwawa hilo lingeweza kutumia zaidi ya Hekari 15.

Kufuatia hali hiyo,Nsumba alisema kama serikali itakubali masharti yake, bwawa hilo lichimbwe lakini iwe mali yake binafsi, kuliko kuchimba kwa manufaa ya Kijiji, hivyo alimuambia Mbunge huyo, hatoi tena eneo hilo na mradi huo wauondoe kwenye kijiji hicho.

Kauli hiyo iliungwa mkono na wanakijiji wenzake, ambapo  Saambili Lukubanija,alisema pamoja na kwamba mradi huo ulipitishwa lakini jamii nyingi haikushirikishwa,hivyo na yeye aliungana na Nsumba, kuitaka serikali iuondoe mradi huo kwenye kijiji hicho.

Kabla ya hapo, Diwani wa kata hiyo,Yuda Majonjo,alisema wananchi hao walipitisha mradi huo wa bwawa ujengwe kwenye kijiji hicho, na tayari fedha zimeishaingizwa, hali ambayo alidai hata naye inamshangaza kwa wananchi hao kukataa mradi huo.

MBUNGE Kwandikwa akitoa ushauri katika eneo la Nsumba.



Majonjo alisema, wananchi hao waliupitisha mradi huo kwa taratibu zote za sheria za vijiji kwenye Mkutano, na kuongeza kwamba baada ya hapo  waliingia wanasheria wa mitaani ambao waliwapotosha wananchi hao, hali iliyosababisha kukatawaliwa kwa mradi huo.

Nae Mbunge wa Jimbo la Ushetu,Kwandikwa,alisema hawezi kuwalazimisha wananchi wa kijiji hicho, kupokea mradi huo isipokuwa aliwataka wakatae kwa kufuata taratibu zote za Serikali ya Kijiji, ikiwa na pamoja na kuitisha Mkutano Mkuu ili wananchi waweze kushirikishwa.

“Kama mmedhamiria kuukataa mradi huu,sintoweza kukulazimeshini,isipokuwa nakuombeni basi mfuate taratibu kama za awali wakati mnauafiki,itisheni Mkutano  Mkuu wa Kijiji, kisha muandike muhtasari ukiwa ni pamoja na mahudhurio yote kisha tuupeleke sehemu husika kama tulivyopeleka wakati wa kuupokea mradi huo,”alisema Kwandikwa.

Mradi huo wa bwawa ulikuwa umeandaliwa kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza kupitia Shirika la OXFAM,kwa lengo la kutumika kwenye kilimo cha Umwagiliaji na tayari katika maeneo mengine wilayani Kahama,mradi huo umepokelewa na utekelezaji wake umeishaanza.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI