Monday, February 29, 2016

TMF IKO TAYARI KUGHARAMIA MATANGAZO YA TBC BUNGENI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




HATIMAYE kilio cha Watanzania kilichojitokeza baada ya Serikali kusitisha matangazo ya moja kwa moja kutoka Bunge la Tanzania kupitia Shirika la Utangazaji nchini (TBC),kwa madai ya  ukosefu wa fedha,kimepata ufumbuzi.

Suluhisho hilo kwa Watanzania limetoloewa na Mfuko wa Vyombo vya Habari nchini (TMF),lililodai kuwa tayari kurejesha haki hiyo ya msingi kwa Wananchi kwakuwa tayari  kutoa fedha zinazohitajika na TBC.

Akiongea hivi karibuni na Wahariri wa Vyombo vya Habari,Jijini Dar Es Salaam,Mkurugenzi Mtendaji wa TMF,Ernest Sungura,alidai pindi Serikali itaafiki pendekezo lao,wananchi wataendelea kunufaika na vikao vya moja kwa moja vya bunge,na si utaratibu ilioanza wa kunakili baadhi ya sehemu na kisha kuoneshwa usiku.


Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TMF,aliwaeleza wahariri wa habari na serikali kupitia mwakilishi wake Assah Mwambene ambaye ni Mkurugenzi wa Habari Maelezo kwamba, taasisi hiyo imejipanga kutoa gharama inayohitajika ili kuhakikisha Watanzania wanaendelea kupata matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni kupitia TBC.

Sungura alisema taasisi hiyo imaemaua maamuzi hayo kutokana na kwamba miongoni mwa malengo ya mfuko huo ni pamoja na kuleta mabadiliko katika tasnia ya habari,nchini kwa  kuhakikisha wananchi wanapata taarifa kwa wakati.


Januari mwaka huu, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,Nape Nnauye, alitoa ufafanuzi bungeni kuhusu hatua ya serikali kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya bunge kupitia TBC,huku akianisha sababu alizozieleza ni pamoja na kuwepo kwa gharama kubwa katika kurusha matangazo hayo.

Nnauye alisema gharama ya Sh. 4.2 bilioni zinazotumika katika uendeshaji wa matangazo hayo ya moja kwa moja kwa mwaka,huku kuwepo kwake kukidumaza ufanisi wa shughuli maofisini kutokana na  watumishi wa serikali kushabikia bunge badala ya kuendelea na kazi ofisini.


Hatua ya serikali kusitisha matangazo hayo iliibua mjadala mkubwa bungeni huku Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo) akilitaka bunge kusitisha shughuli zake ili kujadili taarifa hiyo ya serikali.

Nje ya bunge mjadala huo uliendelea bila kupatikana kwa ufumbuzi ambapo TMF imedhamiria kugharamia matangazo hayo ili kuruhusu wananchi kuendelea kupata matangazo hayo kupitia TBC.

Katika mkutano huo, Mwambene amesema kwamba, serikali itafikiria namna ya kupeleka maombi TMF ya uwezeshwaji katika maandalizi ya miswada miwili ya sheria za habari ili kupitisha sheria zenye matakwa ya wadau.

Kuhusu hilo, Sungura amesema taasisi yake iko tayari kuisaidia serikali kwenye mchakato huo na hata kuitisha kongamano kubwa la wadau.



KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI