Thursday, March 3, 2016

BINTI WA ODINGA AOMBA RADHI WATANZANIA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




MTOTO wa Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga, Rosemary amewaomba radhi Watanzania kwa kauli yake kwamba Olduvai Gorge iko nchini humo.

Maudhi hayo yalisababisha kuibuka kwa mijadala katika mitandao ya Kijamii,kwa Watanzania kujitokeza kumshutumu mtoto huyo wa Waziri Mkuu wa zamani wa Taifa hilo la Kenya.  

Rosemary Odinga anasema “Nilikosea,nawaomba radhi Watanzania,ukweli Bonde la Oldupai ama Olduvai liko Tanzania, nimekubali kuwa nilikosea nilipokuwa nikihutubia mkutano wa viongozi wa vijana kutoka kote duniani nikiwa New York Marekani(International Young Leaders Assembly).”

 Anaendelea kusema “Nahisi kama ambaye nimewakosea ndugu zangu kutoka Tanzania.Nia yangu ilikuwa ni kusema kuwa nilipokuwa mdogo nikienda shuleni nilifunzwa kuwa fuvu la mtu wa kale lilipatikana Olorgesaiile eneo la Kajiado.”

“Nahisi kama ambaye nimewakosea ndugu zangu kutoka Tanzania.Nisemeje ,,nawaombeni radhi Watanzania.Olduvai Gorge iko salama wala haijanyakuliwa na Kenya.

‘Katika ile hali ya undugu naomba kuwanyoshea mkono wa amani kwa sababu mwisho wa siku Afrika mashariki ndio kitovu cha ubinadamu” alisema bi Odinga kupitia mtandao wake wa Instagram.
Tamko lake kuhusiana na bonde hilo la Olduvai (Oldupai) lililoko Tanzania lilihusiana na mada ya siku hiyo.

‘Katika ile hali ya undugu naomba kuwanyoshea mkono wa amani kwa sababu mwisho wa siku Afrika Mashariki ndio kitovu cha ubinadamu” alisema bi Odinga

Olduvai ndiko kulikopatikana vifaa vilivyotumika na watangulizi wa binadamu yapata miaka milioni moja na laki sita iliyopita (milioni 1.6)

Bi Rosemary aliomba radhi baada ya kuzomewa na maelfu ya watu kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook Instagram na Twitter wakidai aliwapotosha hadhira yake na haswa ulimwengu kwa kusema eti Olduvai ipo Kenya.

Kwa upande wake,Mbunge Zitto Kabwe alikuwa amechangia mada kwa kusema kuwa Tanzania sharti izinadi vivutio vyake vya kitalii ilikuzima dhana potovu.

Aidha alidai kuwa watu wanafikiria kuwa mlima Kilimanjaro uko Kenya ilhali ukweli halisi upo Tanzania sawa na mwanamuziki nyota Diamond Platnumz ambaye ni Mtanzania.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI