Wednesday, February 17, 2016

ZAIDI YA WANAFUNZI 500 WA DARASA LA KWANZA WANAKAA CHINI USHETU

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

WAKATI Rais  John Magufuli,akisisitiza kuuwajibisha Uongozi wa eneo lolote nchini kwa uzembe wa Shule kukosa madawati,imeelezwa  zaidi ya Wanafunzi 500 wa darasa la kwanza katika shule ya Msingi  Ulowa,Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu Wilayani Kahama,wanaketi chini.
 
Akiongea na Gazeti hili Diwani wa Viti Maalumu kutoka katika Kata ya Ulowa,Gabriela Alphonce, alisema  mbali na ukosefu huo wa madawati pia kuna upungufu wa madarasa hali inayolazimu wanafunzi kusomea katika vyumba viwli vilivyotengenezwa kwa maturubai.
 
Diwani huyo alisema mazingira hayo ya shule yanavunja hali wazazi ambao wamekuwa wakijitahidi kuhakikisha vijana wao wanapata sare nzuri za shule pamoja na Madaftari,hivyo kuitilia shaka sera ya kupata elimu bure kama itakuwa na ufanisi kwa Taifa .
 
 
 Aidha  alisema kuwa  Wanafunzi hao wa Darasa la kwanza   wapo 609 huku wasichana wakiwa  303 na wavulana 307  na kuongeza kuwa shule hiyo pia ina vyumba vinane tuu vya madarasa ambavyo vinatumika kwa sasa huku mahitaji halisi yakiwa ni vyumba 25.
 
Pia Diwani huyo aliendelea kusema kuwa katika shule ya Msingi Kangeme pia kuna upungufu wa Matundu 62 ya vyoo huku matundu manne tuu yakitumiwa ma Wanafunzi wa shule hiyo hali ambayo inafanya Wanafunzi wengine kujisaidia Vichakani.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, Isabela Chilumba,katika Kikao cha baraza la Madiwani ,alikiri kuwepo kwa hali hiyo katika shule hizo na kuongeza Halmashauri yake imejipanga katika kujenga Vyumba viwili vya madarasa katika shule ya Msingi Ulowa ili kuweza kupunguza mrundikano wa wanafunzi darasani.
 
“Kweli Halmashauri yangu inakiri kuwepo kwa wimbi la Wanafunzi zaidi ya 500 wa darasa la kwanza katika shule ya Ulowa na hii inatokana na mwitikio wa wazazi kuwapeleka wanafunzi shule kwa mwaka huu na changamoto inayotukabili sisi kama Halmashauri ni kuhakikisha kuwa vumba vya madarasa vinajengwa”, Alisema Isabela Chilumba.
 
Aidha alisema kuwa wazazi wamejitokeza katika kuwaandikisha wanafunzi elimu ya msingi na kuongeza kuwa Halmashauri yake haiwezi kuwarudisha wanafunzi majumbani kwa kuwa tayari wazazi walishaghramika kuwanunulia mahitaji muhimu ya shule Wanafunzi  hao.
 
Aidha aliendelea kusema kuwa kwa Upande wa Shule ya sekondari Halmashauri yake tayari imeshatatua changamoto zilizokuwepo ikiwemo upungufu wa madawati hali ambayo tatizo zilimebaki katika baadhi ya shule za Msingi zilizopo katika Halmashauri hiyo mpya.
 
 
Rais Magufuli alirejea  kauli yake hiyo,wakati akiongea na baadhi ya wazee wa Dar Es Salaam,kwa kuonya kutowajibika ipasavyo kutasababisha serikali yake kutoendelea kuwaonea aibu bali itaendela kutumbua majipu .
 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI