Thursday, February 18, 2016

TAMISEMI NAYO YATUMBUA MAJIPU

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



SERIKALI ya Awamu ya Tano imeweka mkazo katika kutumbua majipu,kadri ya maagizo ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,John Magufuli aliyotoa na kuahidi katika hotuba yake ya kwanza,kwa safari hii  Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais{TAMISEMI} kutengua uteuzi wa Mkurugenzi.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais{TAMISEMI},George Simbachawene,ameendeleza utamaduni huo kwa kuamua kutengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mji wa Tunduma,Halima Mpita kwa kumsimamisha kazi kutokana na matumizi mabaya ya madaraka.

Mpita anatuhumiwa kwa upotevu wa mapato ya Serikali,yanayotokana na ushuru wa magari yanayosafari nje ya nchi kupitia mpaka wa Tunduma sambamba na kuwaingiza kazini watoto wake kinyume cha sheria na kuwalipa posho.

Baada ya kutengua uteuzi huo,alimteua,Erick Mapunda,aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu katika Jiji la Mbeya,kukaimu wadhifa huo.

Mbali na Mkurugenzi huyo,pia utumbuaji majipu uliwafikia Wakurugenzi watatu wa Halmashauri za Mbogwe,Misenyi na Nanyumbu sambamba na Ofisa mmoja wa Halmashauri ya Kilolo,kwa tuhuma za kuwarubuni na kutoa rushwa kwa maofisa wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali{CAG},ili hati za Halmashauri zao ziandikwe vizuri.

Waziri Simbachawene anasema Wakurugenzi hao kwa nyakati tofauti mwaka jana Wakurugenzi hao walitoa fedha kuwapa maofisa wa CAG,wwakati wakitekeleza wajibu wao wa kukagua Halmashauri hizo.

Amemtaja,Elizaberth Kitundu,aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Misenyi,Mkoani Kagera,kuhusika na kufanya jitihada hizo kwa kumtuma Mweka Hazina wake,Majaliwa Biakwaso kutoa Sh.3 Milioni kwa maofisa wa CAG kusudi wafiche kasoro walizobaini.

Aidha kwa upande wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Nanyumbu,mkoani Mtwara,Alli Kasinge kupitia kwa Mweka Hazina wake,Paschal Malowe na Mhasibu wa Halmashauri hiyo,Emmanuel Mugesa,walimpatia Fedha kiasi cha Sh.3.5,Ofisa wa CAG,F.Mwampashi,kwa niaba ya wenzake ili waandike Hati safi.

Katika Halmashauri ya Mbogwe,Mkurugenzi wake,Abdallah Mfaume na Mweka Hazina wake,Lucas Elias walitoa Sh.16 Milioni kwa maofisa watatu wa CAG ili kuficha madhaifu yaliyojitokeza katika Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe,ikiwemo matumizi mabaya ya fedha kiasi cha Sh.200 zilizofanywa pasipo nyaraka.

Pia Sh.144 Milioni kulipwa kwa Mkandarasi pasipo kufanyika kazi iliyokusudiwa,sambamba na kubainika malipo ya Mishahara ya Watumishi 82 kufanyika huku wakiwa tayari wameishahama katika Halmashauri hiyo.

Kwa upande wa Halmashauri ya wilaya ya Kilolo,mtumishi wa Idara ya Fedha,Lackson Pina,alitumia kiasi cha Sh.200,000/= kumpatia Ofisa wa CAG kwa malengo ya kulinda mapungufu yaliyojitokeza katika Halmashauri hiyo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI