Monday, February 15, 2016

TASAF III KAHAMA YAWANUFAISHA WASIO WALENGWA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalim
BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Mji wa Kahama,limeiagiza Mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF III wilayani Kahama,kusitisha misaada inayotoa badala yake irudie upya kuzitambua Kaya maskini,kutokana na huduma wanayotoa hivi sasa kuwanufaisha wasio walengwa.  
 
Agizo hilo lilitolewa juzi katika Kikao  cha Baraza hilo baada ya Diwani wa Kata ya Malunga,Shaban Selle,kubainisha zoezi zima la kutambua Kaya maskini katika Kata yake halikufanyika kwa ufanisi na Viongozi wa TASAF III kwa kutoweza kuwafikia walengwa hali badala yake kunufaisha jamii yenye uwezo.
 
Diwani huyo,Sele,alisema Mfuko huo umekuwa ukiendelea kutoa fedha kwa Kaya ambazo hazistahili na kusababisha kuwepo manung’uniko katika jamii hivyo kuona ni vyema ukafanyika upembuzi yakinifu kubaini Kaya maskini zinazostahili kunufaika na Mfuko huo.
 
Madiwani wengine wa Kata za Kahama Mjini,Majengo na Nyasubi walidai manung’uniko hayo pia yanapatikana katika Kata zao huku wakikosa ushirikiano wa kutosha kutoka kwa viongozi pindi wanapowaomba kupatiwa orodha ya majina ya walengwa katika Mfuko huo.
 
Aidha Madiwani hao walishangazwa kuona usiri unaofanyika katika kuhudumia Kaya hizo maskini kwa viongozi wanaosimamia Mfuko huo kwa wilaya nzima kutowashirikisha Waandishi wa Habari katika majukumu yao wakati wanafahamu wanastahili kufanya hivyo hasa kwakuwa kuna baadhi ya waandishi walipatiwa semina na Mfuko huo.
 
Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kahama,Abel Shija, alisema ili kuondoa manung’uniko hayo na kuhakikisha Kaya maskini zinazostahili kunufaika na Mfuko huo ambazo kwa kipindi hiki hazijanufaika ni bora huduma hiyo ikasitishwa kwa muda na kufanyika upembuzi yakinifu kwa wakati ndipo huduma iendelee kutolewa.
 
Alisema kuwa watu wamekuwa wakigawana fedha ambao hawana sifa na pia kuna wengine wakitoka kata nyingine kwenda nyingine kupata msaada huku wakisingia kuwa wao ni waathirika wa ugonjwa hatari wa Ukimwi hali ambayo mfuko huo umekuwa kwa ajili ya kunufaisha watu wachache.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Anderson Msumba alisema kuwa ni kweli mfuko huo umekuwa na mapungufu na kuongeza kuwa zoezi la kutambua kaya masikini linasimamiwa na kamati za Vijiji na kata katika maeneo yanayohitaji msaada.
 
Hata hivyo    alisema kuwa dosari hizo waliishazibaini kutokana na  zoezi la awali la kuwatambua kutofanyika kwa ufasaha na marekebisho kupitia viongozi wa Mfuko wa Tasaf awamu ya tatu inaendelea kufanyika kutambua Kaya maskini zinazostahili huku wakihakikisha ambao tangu awali walistahili kupata huduma hiyo wakiendelea kupatiwa. 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI