Tuesday, February 23, 2016

YANGA,SIMBA ZAREJESHA UTANI WA JADI KWA MASHABIKI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



NANI  anasema soka la Tanzania halina mvuto ama ushabiki?Pamoja na Watanzania kubobea katika upenzi wa soka la Uingereza,lakini ushabiki wa soka la hapa nchini bado una nafasi hasa kwa Watani wa Jadi,Yanga na Simba.

Pambano la Yanga na Simba lilikuwa likisubiriwa kwa hamu kubwa ambapo Yanga iliyokuwa imejificha Kisiwani Pemba,na Simba mji kasoro bahari,huku likiwaacha mashabiki wake sambamba na viongozi wao na chembe chembe za hofu,lilimalizika kwa Yanga kuendeleza ubabe kwa watani zao kwa msimu kwa kuwapachika bao 2 – 0.

SHABIKI wa Yanga,Chuma Muuzakahawa,akimnywesha soda Shabiki wa Simba,Shija Kinga mara baada ya kumvisha skafu ya Yanga na kumkabidhi matunda na mboga za majani,huku mashabiki wengine wa Yanga wakimkabidhi mboga za majani,Mussa Zengo,sambamba na kumpamba kwa bendera ya Yanga,vitendo hivyo vilifanyika katika eneo la Isaka Station.
Inafahamika kwamba mechi ya watani hao ni kubwa na yenye ushawishi mkubwa barani Afrika huku ikishikiria na nafasi ya tatu,na kwa ukanda wa Afrika Mashariki ikiwa ndio kinara ambapo imedhihirisha hilo kutokana na ushabiki ulioambatana na utani mkubwa miongoni mwa mashabiki wa timu hizo.

Utani huo wa jadi ambao ulionekana kupotea kwa fikra za kutekwa na soka la Uingereza,umeonekana kurejea kwa kasi kubwa hususani katika Mji Mdogo wa Isaka baada ya mashabiki wa timu hizo kufanyia utani mara baada ya pambano hilo kukamilika.

Mashabiki hao walioamua kuketi eneo moja na kushuhudia pambano hilo kupitia king’amuzi cha Azam,baada ya pambano mashabiki wa Yanga wakiongozwa na Gambalala Daud waliwafanyia utani wenzao wa Simba kwa kuwanunulia vyakula vyenye rangi za njano na kijani na kuwakabidhi.

Mbali ya kuwanunulia vyakula hivyo,pia waliwanunulia soda zilizokuwa za njano na kuwanywesha,kisha walianza kuwapitisha katika mitaa kadhaa ya Mji huo maarufu kwa jina la Bandari ya nchi kavu,kisha waliwaongoza hadi katika kaya zao na kuwakabidhi katika familia wanazomiliki.

SHABIKI wa Yanga,Gambalala Daud,mwenye Kibaghalashia,akimkabidhi mboga na matunda shabiki wa Simba,Shija Kinga,akimtaka aanze kula majani kwakuwa hana meno tena ya kutafuna nyama.
Mashabiki hao wa Simba walibezwa mbele za wake zao kuwa wao ni wanawake kwa Yanga,na kwamba wameolewa ndoa ya kudumu ndio maana Yanga anafunga kadri atakavyo,hivyo kwa kuwa wao mashabiki hawana budi kutambua kuwa mashabiki wa Yanga ndio mabwana zao,hivyo kushinikiza vyakula walivyowanunulia kuviingiza majumbani kwao tayari kwa kupika na kuvitumia.

“Ninyi ni wake zetu hivi vyakula tulivyowanunulia tumetimiza wajibu wetu kama wanaume,chonde chonde msijifanye vidume kuwashurutisha wake zenu kuvipika,ingieni jikoni ninyi wenyewe na sasa hivi vipokeeni na kuviingiza ndani,”alisema Gambalala kwa mmoja wa mashabiki wa Simba,Shija Nkinga ambaye alipokea na kuingiza ndani mwake.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI