MCHEZAJI
Nguli wa soka katika timu ya Simba Sport Club,ambayo mwishoni mwa wiki ilipokea
kipigo cha bao 2 – 0 kutoka kwa watani zake Dar Yanga African,Mwinyi
Kazimoto,amekana shitaka linalomkabili la kumshambulia na kumdhuru mwandishi wa
habari za michezo wa hgazeti la Mwanaspoti.
Kazimoto
alikana shitaka hilo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Shinyanga
mara alipopandishwa kizimbani kwa kosa la kumshammbulia na kumdhuru mwili
mwandishi wa wa kampuni ya
Mwananchi Communications Ltd, Mwanahimba Richard.
Akisomewa shitaka hilo mahakamani hapo na mwanasheria
wa serikali,Upendo Shemkole alisema mshitakiwa alitenda
kosa la shambulizi la kudhuru mwili Februari
10/2016, katika uwanja wa CCM kambarage baada ya
mazoezi alionekana kumshambulia mwandishi wa
habari Mwanahimba Richard.
Hata
hivyo mshitakiwa Mwinyi Kazimoto baada ya
kusomewa shitaka hilo alikana kutenda kosa hilo ,
na kuiomba mahakama kumpatia mwezi mmoja ili
atafute wakili wa utetezi wake ombi
ambalo lilikubaliwa.
Hakimu
mkazi , mfawidi wa mahakama hiyo Rahim Mushi
anayesikiliza kesi hiyo alisema
imeahirishwa hadi March 21 mwaka, huu
ndipo itaendelea tena kusikilizwa ili kutoa fursa
kwa mshitakiwa kupeleka wakili wake wa utetezi.
Jumla
ya mashahidi sita wanatarajiwa kutoa ushahidi
mahakamani hapo katika kesi hiyo inayomkabili kiungo mchezaji
wa Simba Mwinyi Kazimoto, ambapo pia
alipatiwa dhamana sh 500,000 na mwanasheria wa
halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Batromeo
Lwela.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI