Mabao ya Mabingwa hao
watetezi yalipachikwa kimiani mnamo dakika ya 39 ya mchezo na Donald Ngoma raia
wa Zimbabwe,huku bao la pili likifungwa na raia kutoka Burundi,Hamis Tambwe
mnamo dakika 72 ya mchezo.
Katika pambano hilo
la Watani wa Jadi linaloshikiria rekodi ya tatu Afrika kwa mechi za Mahasimu,likitanguliwa
na National Al-Ahaly na Zamaleck za Misri,zinazofuatiwa na Tunis Express na
Raja Casabranka za Tunisia,na nafasi ya 20 Duniani,mnamo dakika ya 25,katika
faulo ambayo haikuwa kubwa,Mwamuzi wa mchezo, Jonesia Rukiya alimlamba Kadi ya
pili ya Njano kisha kumtoa nje kwa Kadi Nyekundu Abdi Banda wa Simba,kwa
kumwangusha Ngoma.
Aidha
baada ya Mtanange huo,mshambualiaji wa Kimataifa wa Yanga,Amis Tambwe,alisema
pambano hilo lilikuwa la ushindani na kilichowponza Simba na kuwa faida kwa
tiimu yake ni kutolewa kwa Kadi Nyekundu kwa Banda.
Hata
hivyo alisema Simba walijitahidi kucheza vizuri licha ya kuwa pungufu,na
kujinasibu kuwa timu yake ya Yanga ilikuwa bora zaidi katika mchezo huo ndio
maana imeibuka na Ushindi wa bao 2 -0 kama ilivyokuwa katika mchezo wa kwanza.
Yanga katika mchezo
huo iliwakilishwa na Ally Mustapha ‘Barthez’,Juma Abdul,Haji Mwinyi,Pato
Ngonyani,Vicent Bossou,Mbuyu Twite,Deus Kaseke{Geofrey Mwashiuya dak 64},Thabani
Kamusoko, Amissi Tambwe,Donald Ngoma na Haruna Niyonzima{ Simon Msuva dak 53}.
Nayo
Simba iliwakilishwa na;Vicent Agbani,Hassan Kessy,Mohammed Hussein ‘Tshabalala’,Juuko
Murshid,Abdi Bhanda,Justuce Majabvi,Mwinyi Kazimoto{ Novat Lufunga dak 46},Jonas
Mkude,Hamisi Kiiza{ Danny Lyanga dak 59},Ibrahim Ajibu{ Bryan Majwega dak 80}
na Said Ndemla.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI