MHESHIMIWA Gerlad Mwanzia. |
MWENYEKITI
wa kamati ya Elimu, Afya na Maji,
Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama,mkoani Shinyanga,Gerlad Mwanzia amefanya ziara ya kushtukia katika baadhi ya
shule zilizopo katika kata ya Isaka kujionea maendeleo na changamoto zilizopo
katika shule hizo.
Mwanzia
ambaye pia ni diwani wa Kata ya Isaka alifanya ziara hiyo jana,katika
Shule za Msingi Bandari na Isaka pamoja
na
Shule ya Sekondari Isaka.Ambapo awali alifika katika Ofisi za Kata majira ya
saa 1:34 na kulazimika na kuondoka na Kitabu cha Mahudhurio ya Watumishi.MH:Mwanzia akiondoka na kitabu cha mahudhurio |
Diwani
huyo aliamua kuondoka na Kitabu hicho kutokana na kuchelewa kwa watumishi
katika ofisi hiyo,ambapo alikuwepo Mgambo tu ambaye ndiye alifungua ofisi
hiyo,kitendo kilichomchukiza kwakuwa alidai ni kero na kinachelewesha kutoa
huduma kwa wananchi kwa wakati.
“Wananchi
wanahitaji kuhudumiwa matatizo yao kwa wakati,wao wanachelewa ina kera ni vyema
waache kufanya kazi kwa mazoea,awamu hii tunahitaji uwajibikaji uliotukuka ili tupate
maendeleo stahiki,kitendo hiki nitakifikisha kwa mwaajiri wao ambaye ni
Mkurugenzi,”Alisema Mwanzia.
Akiwa
katika Shule ya Msingi Bandari alishuhudia
idadi kubwa ya walimu wakichelewa kufika shuleni katika muda wa
kazi na kulazimu kumwagiza mwalimu Mkuu
wa Shule hiyo Pili Hamisi ampatie taarifa ya maelezo ya walimu kwanini
wamechelewa ifikapo Jumatatu.
WANAFUNZI wakiendelea na masomo. |
Hata
hivyo Mwanzia alijionea changamoto
mbalimbali katika shule hiyo,ikiwemo upungufu wa madawati,hali ambayo inalazimu
wanafunzi kukaa chini pamoja na uhaba wa matundu ya vyoo hali ambayo inatishia usalama wa afya za
wanafunzi.
Mwalimu
Mkuu wa shule hiyo,Pili Hamisi alisema
ipo mikakati ambayo wameanza kuifanya ili kunusuru hali hiyo,hususani
katika suala la mapungufu la madawati kwa kutumia fedha zilizochangwa na jamii
kwa ajili ya maendeleo ya shule .
AKIANGALIA Dawati zinazotakiwa kufanyiwa ukarabati |
Kwa
upande wake Mwanzia alisema ni vyema changamoto zinazoweza kutekelezeka kwa wakati
pasipo kusubiri msaada kutoka serikalini ukafanyika ili kuinusuru Shule hiyo,na
kusisitiza suala la uzalendo kwa walimu katika kusimamia changamoto hizo.
Aidha
katika shule ya sekondari Isaka, matokeo
mabaya ambayo shule hiyo
imeyapata ya kidato cha nne yameonesha
kumshitua diwani huyo, kutokana na
kwamba shule hiyo imefaulisha wanafunzi
19 pekee kujiunga na kidato tano
huku wanafunzi 62 wamepata wasitani wa
daraja la sifuri.
“Matokeo
haya si mazuri,ni vyema mkaketi mkatafuta chanzo cha tatizo,hamstahili
kulaumiana.Mkipata kiini chake ndipo mtapopata ufumbuzi wa kutatua na
kuondokana na shule kufanya vibaya,”alisema Mwanzia.
Mkuu
wa shule hiyo,Daniel Kabola alieleza changamoto zilizosababisha hali hiyo,kuwa
ni kutokana na utoro mkubwa uliokithiri wa wanafunzi huku jamii ikiwa na
ushirikiano mdogo katika kukabiliana na hali hiyo.
Kabola
alisema kuna wanafunzi wanatumikishwa na walezi wao kufanya biashara hadi
nyakati za usiku hali inayoathiri uwezo wa kufanya vyema katika masomo kwa
vijana hao,huku baadhi ya watoto wa kike wakijitumbukiza katika masuala ya
mapenzi kwa ushawishi wa madereva wa magari makubwa ya mizigo yapelekayo bidhaa
nchi jirani za Rwanda,Burundi na Kongo.
Nae
Mwalimu wa Taaluma katika Sekondari hiyo,Violet Cyprian alisema wanafunzi
hawapati fursa ya kurejea waliyofundishwa shuleni wakiwa nyumbani kutokana na
kutumikishwa shughuli mbalimbali,jambo linalosababisha vijana kushindwa kufanya
vizuri katika masomo yao.
Hata
hivyo walimu hao walisema baada ya Matokeo hayo kuwa mabaya wamejipanga kufanya
vyema ili kunusuru hali hiyo kwa kuhakikisha wanafundisha kwa bidii zaidi na kuongeza
muda wa ziada kwa kuwaweka wanafunzi katika makundi ya mijadala na kuwapatia
mazoezi zaidi ya masomo mbalimbali.
Chanzo
chetu ni Boniphace Mabisilo
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI