Sunday, February 28, 2016

WATOTO CHINI YA MIAKA KUMI WANG’OLEWA MENO KAHAMA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


IMEFAHAMIKA jamii kupenda vyakula vyenye sukari nyingi huku ikikosa Elimu ya Kinywa na Meno,ndio chanzo cha watoto wengi wenye umri chini ya miaka kumi,kung’olewa meno,na asilimia 90 wenye zaidi ya  miaka 30 kutokuwa na meno 32.
 
 
Hayo yalielezwa na Mratibu wa Mafunzo ya Kinywa na Meno kutoka Shirika lisilo la Kiserikali la Bridge2Aid,Innocent Bikere,ambapo alibainisha hali hiyo inawaathiri kwa kiwango kikubwa jamii inayoishi vijijini,kutokana pia kutopatikana huduma ya kinywa na meno kwa wakati.
 
 
Bikere alisema jamii ya vijijini inapenda kutumia vyakula na vitu vyenye sukari nyingi huku kwa kipindi cha zaidi ya miaka 15,ikiwa haina utamaduni wa matumizi ya mswaki kwa ajili ya afya ya vinywa vyao,hivyo kusababisha kuwa na matatizo ya meno yao kuuma na mengine kuoza. 
.
 
Alisema Shirika lake lenye makao makuu yake jijini Mwanza,baada ya kufanya utafiti na kuona Wizara ya Afya haiweki kipaumbele katika Huduma ya kinywa na meno,liliomba ufadhili katika kampuni ya ACACIA kupitia Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu na kufanikisha kutoa meno watu 800 huku asilimia 30 ikiwa ni watoto chini ya miaka kumi.
 
 
Kwa upande wake Dk. Helen Young, kutokana nchini Uingereza ambaye ameongoza jopo la Madaktari 12 kutoka nchi hiyo, alisema lengo lilikuwa kutoa Elimu ya usafi wa Vinywa kwa Matabibu katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama.
 
 
Dk. Young alisema katika mafunzo yao kwa vitendo waliwahitaji wananchi wenye meno mabovu wafike kwenye vituo vilivyopangwa vya Lunguya na Bugarama, kupata Elimu hiyo ya Usafi wa Vinywa na kuwapatia tiba kwa meno yaliyotoboka,lakini walilazimika kung’oa baada ya kubaini  yameoza.
 
Nae Meneja wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu,Graham Crew alisema kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Kampuni ya ACACIA,imefadhili mradi huo ili kuwasogezea huduma hiyo wananchi wanaoishi katika maeneo yaliyo jirani na Mwekezaji huyo,ili kupatiwa huduma ya matibabu ya meno.
 
 
Katika zoezi hilo, jumla ya Matabibu 6 katika Halmashauri ya Msalala wamepatiwa mafunzo ya huduma ya Kinywa na wakati wa mafunzo hayo, idadi kubwa ya wananchi waliofika kupewa Elimu hiyo walibainika meno yao yameoza kutokana na utunzaji hafifu wa kinywa.
 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI