Friday, February 26, 2016

WASANII WAIDAI MAMILIONI IKULU

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



KATIBU Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue.
IKULU ya Rais Dk.John  Magufuli imeingia katika mgogoro na wasanii wa sanaa za uchoraji baada ya kudaiwa kushindwa kulipa deni lao la Sh.Milioni 53.6.

Wasanii hao 19 wanadai deni hilo lililtokana na kazi waliyoifanya ya kuchora picha mbalimbali ambazo zinapamba Ikulu,walizopeleka Agosti mwaka jana  wakati Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akiwa madarakani.

Wasanii hao na kiasi kianchodaiwa na kila mmoja kwenye mabano ni Cuthbert Semgoja{Sh.Milioni 6.8},Florian Kaija{Sh.Milioni 3},Evarist Chikawe{Sh.Milioni 2.8},Haji Chilonga{Sh.Milioni 6.6}Robino Ntila{Sh.Milioni 3.6}na Vita Malulu{Sh.Milioni8.9}.

Wengine ni Masoud Kibwana{Sh.Milioni 3.5},Said  Ray{Sh.Milioni 1},David Kyando{Sh.Milioni 2},Paulo Ndunguru{Sh.Milioni 1.5},Thobias Minzi{Sh.Milioni 4.1},Lutengano Mwakisopile{Sh.Milioni 1.2}Yussuf  Khamis Yussuf{Sh.Milioni 1.6}na Ali Ali Kigata{Sh.650,000/-}.

Pia wamo Hamza Mohamed Ausi{Sh.800,000/=},Suleiman Rashid{Sh.Milioni 1.8},Ismail Mbarak Mselem{Sh.800,000/-} na Claud Chatanda{Sh.Milioni 2.2},ambao wote kwa ujumla wanadai Sh.Milioni 53.6.

Katika harakati za kudai haki yao,wasanii hao wamesema wamekuwa wakifanya juhudi za kukutana na viongozi mbalimbali wa Ikulu tangu wakati wa Rais Kikwete hadi sasa chini ya Rais Magufuli bila mafanikio.

Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar Es Salaam,Mwenyekiti wa Wasanii hao,Lutengano Mwakisopile,tangu walipowasilisha kazi zao ni zaid ya miezi tisa sasa,lakini hawajalipwa fedha zao.

Alisema waliahidiwa kulipwa fedha hizo kabla ya Uchaguzi Mkuu mwaka jana,lakini wamekatishwa tama na majibu yasiyoridhisha kutoka kwa wahusika Ikulu.

“Ahadi tuliyopewa ni kwamba tungelipwa kabla ya Uchaguzi mkuu mwaka jana na kumekuwa na mlolongo wa ahadi unaojirudia rudia kwamba malipo yenu yanaandaliwa.Kwa vile mawasilano yetu na Ikulu kuhusu deni letu yamezidi kufifia,tumeona njia bora ni kukutana na vyombo vya habari ili watusaidie kupaza sauti zetu,”alisema Mwakisopile na kuongeza:

“Imefikia hatua simu zetu hazipokelewi na hata ukituma ujumbe mfupi wa maneno hupati majibu.Hatukukata tamaa,tukaamua kwa pamoja tujaribu kupiga simu kwenye Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue,lakini maelezo tuliyopewa yanakatisha tama,mwisho wake hakukuwa na majibu yanayoridhisha hadi leo hii.”

Mmoja wa wasanii hao ambae aliwahi kuwa Mjumbe wa Baraza la Sanaa la Taifa(Basata),ambaye aliomba hifadhi ya jina lake,alisema kama Ikulu isipotekeleza malipo yao wataiburuz mahakamani.

                          Idara ya Maelezo lawamani

Mwenyekiti huyo wa wasanii,alieleza jana walifika katika Ukumbi wa Idara ya Habari(Maelezo)kwa lengo la kutaka kuzungumza na wanahabari,lakini uongozi wa Idara hiyo uligoma kuwapa nafasi.

Alisema walipofika majira ya saa nne kutaka kulipia gharama za ukumbi,walikutana na mmoja wa watendaji wa idara hiyo ya serikali ambaye alikataa kuwapa nafasi baada ya kujua azima ya mkutano wao.

“Kwa kuwa tunafahamiana na baadhi ya waandishi ambao huwa tunafanya nao kazi tukiwa na maonyesho walitushangaa kutuona nje ya Ukumbi wa Maelezo,ndipo wakatuita tukaanza kueleza kilio chetu,”alisema Chikawe na kuongeza:

Lengo letu ni kupata haki yetu ya malipo ya kazi tuliyofanyia Agosti mwaka jana,kila mmoja wetu ana idadi yake ya picha,makubaliano yetu yalikuwa tulipwe fedha kabla ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25,mwaka jana lakini hadi sasa hatujalipwa haki zetu,”alisema.

                                              Ufafanuzi wa Ikulu.

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano – Ikulu,Gerson Msigwa,alikiri kuwapo kwa madai hayo nakuongeza kuwa wasanii hao wapo katika mazungumzo na watu wa manunuzi ili kupitia gharama wanazodai kwa lengo la kujua kiasi halisi wanachodai.

“Ni kweli hayo madai yapo na waliyaleta Novemba mwaka jana,lakini kiwango ambacho walikidai ni kikubwa hakilingani na uhalisia wa deni,”alisema Msigwa.

Alisema Ikulu imeshangazwa na hatua ya wasanii hao kuamua kwenda kwenye vyombo vya habari,huku ikijua fika kwamba suala lao linashughulikiwa.

“Kitendo walichokifanya cha kuwa katika mazungumzo halafu wanatoka kwenda kuzungumza na vyombo vya habari ni cha kusikitisha sana,kwani hata walipomaliza kuzungumza na waandishi leo(jana){Februari 24,2016},walikuja tena hapa Ikulu sasa hatujui wana maana gani.”

Kuhusu deni lao alisema mara baada ya watu wa manunuzi wa Ikulu na wasanii hao kumaliza majadiliano,fedha zao zitalipwa mara moja,kwani Ikulu haiko tayari kumdhulumu mtu.

        Chanzo cha Habari ni gazeti la Tanzania Daima.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI