Thursday, February 25, 2016

MADAWATI YASABABISHA KIZAZAA KAHAMA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Anderson Msumba,awatimua wazazi katika madawati huku akipiga marufuku katika kipindi cha masomo jamii kuyatumia kwenye mikutano na vikao mbalimbali,kwakuwa kitendo hicho ni kinyume na haki anazostahili kupatiwa mwanafunzi.
 
 Kauli hiyo aliitoa katika Kata ya Iyenze,wakati akipokea madawati 60 kutoka Ushirika wa Wachimbaji wadogo wa Isalenge Iyenze Gold Mine wa wilayani Kahama,ambapo alisema ni kinyume cha haki za binadamu kutumia madawati yanayohitajika kutumiwa na wanafunzi kipindi cha masomo.
 
Msumba alisema tabia hiyo imezoeleka kwa jamii kukatisha masomo ya wanafunzi kwa ajili ya kutumia madawati kwa kushughuli zao za kijamii na kutoa agizo kwa Maofisa Watendaji wa Kata kusimamia agizo lake la kuzuia madawati kutumika na wazazi ambao wamekuwa wakaidi kuwatengenezea mazingira bora ya kusoma vijana wao.
 
“Inashangaza wazazi hapa wamekusanyika kuja kushuhudia wahisani wakikabidhi dawati huku wakikalia dawati zilizopo 30 na kusababisha vijana wetu kuendelea na masomo wakiwa wameketi chini kuanzia leo marufuku na ninakuombeni myapeleke madarasani nasi tutasimama kuendelea na jukumu lililo mbele yetu,”alisema Msumba.
 
Aidha  Mkurugenzi huyo alitumia fursa hiyo kumuagiza Afisa Elimu wa Halmashauri ya Mji kuhakikisha shule zote hakuna kutoa madawati nje kwa ajili ya mkutano wowote,huku jamii ikishindwa kuchangia  madawati ili kuwezesha vijana kusoma katika mazingira mazuri yatakayowawezesha kufanya vyema katika mitihani yao.
 
Katika makabidhiano hayo Mkurugenzi wa ushirika wa Isalenge Iyenze Gold Mine,James Belela, alisema waliamua kujikita kutoa msaada wa madawati, kutokana na hali mbaya katika shule za Kata hiyo,ambapo waliamua kutoa dawati 40 katika shule ya Msingi Iyenze na 20 katika Shule ya Msingi  Isalenge.
 
Awali katika hafla hiyo, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo David Joseph, alisema shule hiyo inajumla ya wanafunzi 589 huku ikiwa na dawati 90 hali inayosababisha wanafunzi zaidi ya mia mia tatu kutoka darasa la kwanza hadi la saba kukaa chini,hali iliyosababisha Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Ushirika huo,Pius Gulamse kuahidi kutoa dawati zingine 30.
 
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Ushirika huo,Belela alisema ushirika wake uliguswa na uhaba huo wa madawati katika Kata hiyo ambayo ina rasilimali za madini ya dhahabu,japo kuona tatizo hilo ni la wazazi hivyo kuamua kutoa dawati hizo 60, zilizogharimu milioni 9,200,000/= .
 
Pamoja na msaada huo wa dawati pia Ushirika huo uliamua kutoa  mifuko 100 ya Saruji,huku Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji,Msumba kuamua kutoa Shilingi Milioni 12 baada ya kushuhudia wanafunzi wamekaa chini ya vumbi lililochafua nguo kutokana na kuharibika kwa sakafu,na kiasi kingine kuagiza kutumika kukamilisha ujenzi wa vyoo, uliokwama uliokuwa ukifanyika kwa nguvu za wananchi.
 
 
 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI