Thursday, February 4, 2016

WALIOTAFUNA FEDHA ZA MGODI WA BUZWAGI WAKAMATWA NA POLISI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


HATIMAYE Watumishi Saba katika Halmashauri ya Mji wa Kahama,waliosimamishwa kazi na wengine kuwekwa katika Uangalizi,kutokana na kutuhumiwa kufanya ubadhirifu wa fedha za
ushuru wa huduma, zilizotolewa na Mgodi wa Buzwagi,wamekamatwa na Polisi.

Watumishi hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Uzabuni katika Halmashauri hiyo;Marko Nzengula  ,hivi karibuni walisimamishwa na wengine kuwekwa katika uchunguzi baada ya kutuhumiwa kutumia kwa maslahi yao binafsi kiasi cha zaidi ya Shilingi Milioni 800,zilizotolewa kwa lengo la kutekeleza miradi ya wananchi.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo ,Anderson Msumba,watumishi hao walikamatwa na Polisi siku ya Jumamosi,baada ya Kampuni ya Noble Cliff Construction likiwa na vielelezo vya kua na nyaraka za kupatiwa kazi na halmashauri hiyo  kujitokeza  kudai malipo,ilhali yaliishafanyika huku nyaraka zake zikikosa ulinganifu sahihi na nakala ya Bodi ya Uzabuni.
Kufuatia hali hiyo ilibainika kuwa Bodi ya Zabuni iliipa kazi Kampuni ya  na kuilipa fedha kwa madai ina akaunti katika Benki ya NMB na mkataba yote ilionyesha fedha hizo zitapitia huko,hali iliyopishana na madai ya Kampuni hiyo ya kulipwa fedha kupitia Bank Of Africa BOA.
Baada ya kuwepo mpishano huo wa madai kupishana na mikataba,Msumba alisema alimtuma Mweka hazina wake kwenda kukagua Akaunti hizo na kukuta ile ya BOA,ambayo Kampuni hiyo ilidai ilipwe iliishafungwa siku nyingi na ile ya NMB ambayo ilipitishwa na Bodi ya Zabuni ilikuwa ikimilikiwa na mtu binafsi.
Hali hiyo Msumba alisema kulikuwa na udanganyifu katika zoezi zima la Mchakato wa utoaji wa zabuni hiyo,ambao Bodi hiyo ilitoa zabuni za ujenzi mbalimbali kwenye makampuni hewa,hali iliyosabisha,Mkuu wa Wilaya Vita Kawawa kuunda Kamati ya Uchunguzi iliyogundua ubadhirifu wa fedha hizo Milioni 800 kati ya Bilioni Moja zilizoko kwenye thamani ya Miradi hiyo.
Aidha katika tukio hilo la juzi la kampuni ya Noble Cliff kuonekana ni moja ya makampuni yaliyopewa miradi hiyo na Bodi hiyo ya Zabuni bila kufuata taratibu,wajumbe wote wa Bodi ya Zabuni ya Halmashauri ya Mji wa Kahama walikamatwa mpaka kufikia jana walikuwa Mahabusu katika Kituo kikuu cha wilaya.
Waliokamatwa ni pamoja na Katibu wa Bodi ya Zabuni,Joseph Maziku,ambaye ni Afisa Ugavi pamoja na Wajumbe wake  Kulwa Ntaudyimara ambaye ni afisa utumishi,Annastazia Manumbu,ambaye ni Afisa Elimu Sekondari,mwingine aliyekamatwa ni Joachim Henjewele ambaye ni Mkuu wa Idara ya Ardhi,Elius Mollel ambaye ni Afisa Biashara pamoja na Gervas Lugodisha kutoka Ofisi ya Ugavi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Mika Nyange,alikiri kukamatwa kwa watumishi hao na kuongeza kuwa leo Jumatatu atatoa ufafanuzi zaidi juu ya hatua iliyofikiwa kuhusu tuhuma za watumishi hao,baada ya kuwasiliana na Mkuu wake wa Polisi wa wilaya ya Kahama OCD.
Katika tuhuma hizo Mkuu wa Wilaya ya Kahama,Vita Kawawa,kupitia baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo,ambapo Mwenyekiti wake Abel Shija aliwasiamamisha kazi watumishi watano kwa tuhuma hizo kwa kutumia vibaya Fedha za Mgodi wa Buzwagi wengine ambao walikwishahamishwa  aliamua warejeshwe kujibu tuhuma zao.
Na katika tuhuma hizo zilizopelekea kukamatwa kwa watumishi hao ni baada ya kuanza kupatikana makampuni hewa yaliyolipwa fedha hizo huku mengine mawili yanaendelea kutafutwa ambayo tayari kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Halmshauri hiyo yameishalipwa fedha hizo za Buzwagi.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI