Thursday, February 4, 2016

KAHAMA YASHTUKIA USHURU MDOGO UNAOLIPWA NA ACACIA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


SERIKALI wilayani Kahama imeshtusushwa na mapato madogo yanayoingia katika Halmashauri ya Msalala kutoka Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu,hivyo kuwaagiza madiwani katika Halmashauri hiyo,kufanya utafiti wa
kina kubaini idadi ya makampuni yafanyayo kazi Mgodini,na kustahili kulipa ushuru wa huduma.  
Agizo hilo alilitoa Mkuu wa wilaya ya Kahama,Vita Kawawa,katika kikao cha Baraza la Madiwani baada ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo,Patrick Karangwa,kueleza matarajio ya kukusanya ushuru wa huduma kwa mwezi Julai hadi Desemba 2015,kiasi cha Shilingi Bilioni 1.4 kutoka mgodi huo kadri ilivyokisiwa hawakuyafikia baada ya kukusanya Shilingi Milioni 916.1.
Mkuu huyo wa wilaya,hakuridhishwa na mapato yanayopatikana kwenye Halmashuri hiyo kutoka kwa mwekezaji huyo,na kuwaagiza madiwani waisimamie vyema Halmashauri yao kwa kuona umuhimu wa kuangalia upya takwimu zote za makampuni yaliyomo ndani ya mgodi.
“Madiwani mna dhima kubwa kuishauri serikali na kusimamia mapato ya Halmashuri yenu,msisite kwenda Mgodini kuyabaini makampuni ili mvune kinachostahili,nami nitakuwa bega kwa bega kuhakikisha stahili ya Msalala inapatikana kwa kupata ushuru wa huduma hata kwa kampuni iliyofanya biashara na Mgodi kwa siku moja,”alisema Kawawa.
Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Msalala,Wilayani Kahama,Ezekiel Maige,aliwataka Wawekezaji wa Kampuni ya Acacia inayomiliki Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu kuwa wazi kwa Halmashauri ya Msalala kutoa takwimu halisi ya makampuni wanayofanya nayo kazi,ili kurahisisha Halmashauri yao kupata stahili sahihi ya ushuru wa huduma. 
“Kwa sasa kuna umuhimu wa Halmashauri ya Msalala, kutengeneza makubaliano  baina yao na Mgodi huo ili kuwa na mikataba ya kudumu,ili Wananchi waweze kujua hali   ya kazi za Wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni hiyo,na ili kudhibiti mapato hayo  ni vyema Halmashauri ikawa na ofisi ndani ya Mgodi,”alisema Maige. 
Akiongea kwa Niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala Patrick Karangwa, Mweka hazina wa Halmashauri hiyo Deus Ngeranizya alisema kuwa katika Mgodi wa huo wa Acacia Bulyanhulu kuna jumla ya makampuni 25 yanayofanya kazi katika Mgodi huo hali ambayo ilipingwa vikali na Madiwani wa Halmashauri hiyo.
Hata hivyo Madiwani hao walisema kuwa wanataka kujua jumla ya Makampuni yaliopo katika Mgodi huo ambayo yanafanya kazi na kuongeza kuwa haiwezekani kwa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu kuwa na Makampuni machache kiasi hicho kupita Mgodi wa Buzwagi mbao ni mdogo wenye jumla ya Makampuni 168 yanayofanya kazi katika Mgaodi huo.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu katika Halmashauri ya Msalala Gerald Mwanzia alisema kuwa Kamati yake iliomba mchanganuo wa fedha hizo kutoka katika uongozi wa Acacia Bulyanhulu zilizolipwa na Makampuni yanayofanya kazi mgodini hapo lakini ilishindikana kutokana na uongozi wa Mgodi huo kushindwa kutoa ushirikiano.
Alisema kuwa baada ya kutopata ushirikiano wa kutosha kutoka Mgodini hapo Kamati hiyo haikuridhika na majibu pamoja na idadi ya Makampuni inayodaiwa kuwepo katika Mgodi huo ikiwa ni pamoja na yale yanayofanya kazi katika Bandari ya Nchi kavu ya Isaka ambapo kuna Makampuni zaidi ya 30.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI