Thursday, February 4, 2016

MGANGA WA JADI AUAWA NA MTEJA MWENDAWAZIMU ALIYEKUWA AKIMTIBU.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

JESHI la Polisi wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga,linamshikilia kijana mmoja anayedaiwa kuwa mgonjwa wa akili kwa tuhuma za kumuua mganga wake wa kienyeji aliyekuwa akimnywesha dawa kwa
nguvu katika Kijiji cha Ididi Kata ya Nyamilangano wilayani Kahama.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga,Mika Nyange,alisema tukio hilo lilitokea juzi baada ya Mganga  huyo,Jilumba Mabula {70},kuuawa akiwa katika harakati za kumnywesha dawa,mgonjwa wake huyo,Shibo Joel{20}.
Kamanda Nyange alisema Joel ambaye ni mkazi wa Kwimba Mkoani Mwanza alifikishwa nyumbani kwa mganga huyo na ndugu  zake akisumbuliwa na maradhi ya akili na ugonjwa wa kifafa ambapo alipoanza kupewa dawa aligoma kunywa huku akidai hana ugonjwa wowote.
Aliendelea kusema baada ya Joel kugoma kunywa dawa kwa madai hana ugonjwa wowote ndipo ilipomlazimu mganga huyo kuomba msaada wa watu kumshika mtuhumiwa huyo na kuanza kumnywesha kwa nguvu dawa.
Nyange alisema akiwa katika hatua hiyo Joel alifyatuka mikononi mwa watu waliokuwa wakimshikilia na kuchukua jembe la Mkono lililokuwa jirani na walipokuwa na kumpiga nalo sehemu za shavu la kulia hali iyosababisha Mganga huyo kuvunjika taya na kufariki papohapo.
Aidha Kamanda Nyange,alisema Joel ameshikiliwa na Polisi mjini Kahama katika mahabusu maalumu,kutokana na kuhisi anatatizo la akili kwakuwa kwa mujibu wa sheria ugonjwa wake huo utathibitishwa na daktari baada ya kufikishwa mahakamani .
Baadhi ya watu  katika Kata ya Nyamilangano,wamekilaani kitendo hicho na kwamba kimeacha simanzi kutokana na mganga huyo kuwa msaada mkubwa wa matibabu mbalimbali mbali na magonjwa ya vichaa kwa kutumia tiba za asili.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI