NAIBU Katibu CWT;Ezekiah Oluoch. |
WALIMU
wanaostaafu wameonywa kutokimbilia kufanya biashara za kifahari sambamba na
kununua magari kwa pesa zao za mafao yao,badala yake ni vyema wakanunua ng’ombe
wa maziwa na kujikita katika biashara ya
kuuza maziwa,ambayo itasaidia kuwafanya waendelee kuishi maisha mazuri.
Onyo
hilo lilitolewa katika hafla ya kuwaaga walimu nane waliostaafu katika wilaya
ya Kahama,na Mwenyekiti wa Chama cha Walimu {CWT}katika Halmashauri ya
Ushetu,Juma Nyakanyange,ambapo alisema wastaafu wasipotumia mafao yao vizuri
kwa kufanya biashara wanazomudu watakakuwa na maisha magumu.
Nyakanyange
aliwakumbusha kuwa muda wao mwingi wa maisha wameutumia katika utumishi wa
umma,hivyo kujikita katika biashara kubwa za kumiliki maduka,hoteli ama za
magari hawataweza kutokana na ushindani mkubwa wa kibiashara uliopo unaostahili
kuendana na umri,na kujitumbukiza katika biashara hizo ni kujitakia umaskini.
“Muda
mwingi mmeutumia katika utumishi,ni vyema sasa mkafanya biashara inayolingana na umri wenu ambayo
haitawasababishia maradhi ya BP,na inayostahili ni ng’ombe wa maziwa,na ambao
bado tuko katika utumishi tuanze kujiandaa na maisha ya ustaafu,”alisema
Nyakanyange.
Akiongea kwa niaba ya
Katibu Mkuu CWT Taifa,Mwenyekiti wa chama hicho Mkoani Shinyanga, George
Nyangusu,alisema walimu wengi wamekuwa
wakiishi maisha magumu,mara baada ya kustaafu kutokana na kutokuwa na mpango
mzuri wa matumizi ya fedha za mafao ambazo hulipwa walimu hao
wanapostaafu.
“Ni aibu baada ya kustaafu
kuwa na maisha mabaya ya ufukara wakati
umefanya kazi kubwa ya kulitumikia taifa hili ukiwa mwalimu,hivyo ni vyema
walimu kuanzia sasa walimu wanaostaafu walimalize tatizo hilo kwa kuwa makini
na fedha hizo na wanapaswa kuwa na mpango mzuri wa matumizi yake,”alisema
Nyangusu.
Halfa hiyo ya kuwapongeza
walimu hiyo ilikwenda sambamba na kuwazawadia walimu hao wanane kila mmoja
mabati ishirini yote yakiwa na thamani ya shilingi milioni tatu na laki nne,huku
wastaafu hao wakiomba uwepo utaratibu wa kuwaalika na wenzi wao katika hafla
hizo kutokana na kuwa na mchango mkubwa katika maisha yao ya utumishi.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI