Monday, February 8, 2016

KUKIMBIA KESI KWA MAWAKILI KUNATOKANA NA UCHELEWESHWAJI WA KESI KUKAMILIKA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



IMEBAINIKA kwamba chanzo cha baadhi ya Mawikili katika Mahakama mbalimbali Nchini kukimbia kesi za Wateja wao ambazo walianza kuzisimamia
kunatokana na ucheleweshwaji wa
Mashauri hayo kutotolewa hukumu kwa wakati,na kuwasababishia gharama kuwa kubwa tofauti na malipo waliyolipwa.

Akiongea kwa niaba ya Mawakali katika Kilele cha siku ya Sheria nchini Wilayani Kahama,Wakili Msomi Kelvin Murusuri,alisema kutokana na kesi wanazowatetea Wateja wao mwenendo wake  katika Mahakama kutumia muda mrefu   kumesababisha kipato chao kushuka kwa kuhofia kuwa na mrundikano wa kazi.

Wakili huyo alisema kuwa kitendo cha mashauri mengi Mahakamani kuchelewa kusikilizwa kwa wakati kunachangia kwa kiasi kikubwa katika kupunguza Morali  wao wa kufanya kazi hali ambayo inawakatisha tamaa Wateja wao wanaokwenda kutafuta huduma kwao,huku nao kulazimika kuzikimbia baada ya gharama ya kesi waliyokubaliana na mteja kufikia ukomo huku mwenendo wa kesi ukiwa bado mrefu.

Aidha alisema kuwa kama kesi moja itasikilizwa kwa muda mrefu wanapata hasara kubwa kwani kazi yao hiyo ya kutoa huduma inahitajika kwa wananchi wengi na kuongeza kuwa kwa wao kushinda mahakamani kila siku wanapoteza wateja wengi wanaohitaji huduma  yao.

Awali akisoma taarifa ya Mahakama hiyo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama Vita Kawawa aliyekuwa Mgeni rasmi katika sherehe hizo, Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Kahama,Evodia Kyaruzi,alisema kuwa mahakama yake kwa mwaka jana imejitihadi katika kuhakikisha kuwa mashauri waliokuwa nayo yanasikilizwa kwa wakati.

Kyaruzi alisema kuwa kwa mwaka 2015 jumla ya mashauri 1105 yalisikilizwa na kupatiwa hukumu kati ya 1218 yaliokuwepo ,huku 113 yakibaki kitendo ambacho aliwapongeza Mahakimu pamoja watumishi wa Mahakama hiyo kwa kujitahidi katika kutoa huduma kwa Wananchi katika maeneo mbalimbali ya Wilaya. 
Hakimu huyo aliwataka watumishi wa Mahakama kuwa wazi kwa Wananchi kuhusu kazi wanazozifanya  ili jamii iwe na imani katika uendeshwaji wa kesi zao mahakamani hapo hali ambayo itakuwa ni changamoto kubwa kwa wananchi kuelewa sheria tofauti na ilivyo kwa sasa.

Kwa upande wake,Mkuu wa Wilaya ya Kahama,Vita Kawawa, alisema kuwa katika Wilaya ya Kahama kuna tatizo kubwa kwa baadhi wa Wananchi kutozijua sheria kwa kiwango kikubwa hali ambayo inafanya watu wengi kufika ofisini mwake kutoa malalamiko huku matatizo yao makubwa yao yakiwa ni yale ya kisheria.

Kawawa aliwaonya viongozi kutokuwa sehemu ya  waamuzi ya migogoro ya kisheria  bali waelimishe Wananchi jinsi ya  kupata haki katika sehemu husika hali ambayo itapunguza migogoro iliyopo,ambayo kwa asilimia kubwa inachangiwa na masuala ya  ardhi pamoja na mirathi

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI