VIONGOZI wa dini wilayani Kahama wameziomba Mahakama kutekeleza wajibu wao wa kutoa haki kwa uwazi na
Wakiongea juzi katika hitimisho la siku ya Sheria iliyofanyika kwenye viwanja vya
mahakama ya wilaya ya Kahama,viongozi
hao wa dini za Kiislamu na Kikristo,walisema nchi nyingi duniani amani zao
huvurugika kwa wananchi wake kutopatiwa haki,hivyo kuonya suala hilo lisipewe
fursa nchini.
Sheikh wa wilaya {BAKWATA}wilaya ya
Kahama,Sheikh Omary Damka,aliwakumbusha Majaji na Mahakimu,kuwa shughuli
wanazofanya ni za utumishi wa Mwenyezi Mungu hivyo hawana budi kuwa waadirifu
na kuwa majasiri katika kutenda haki kwa kukabiliana na baadhi ya wanaotaka
kupindisha sheria kwa ukwasi na mamlaka yao.
“Mwenyezi Mungu amekasimu mamlaka
yake duniani kwa viongozi wa dini na serikali,hivyo kwa mnaosimamia sheria mna
dhima kubwa ya kutenda haki kwa uadirifu pasina woga wa kuwaogopa wenye kipato
ili wasio nacho wasinyanyasike,na hapo mtakuwa mmesimamia amani nchini,”alisema
Sheikh Damka.
Kwa upande wake Mchungaji wa Kanisa
la Anglikana wilayani Kahama,Patrck Kulije,aliwaomba watumishi wa mahakama waepuke vishawishi na kuzingatia upendo amabao
ndio utakuwa dira ya kutekeleza majukumu yao kwa uadirifu na uwajibikaji
uliotukuka hivyo kuwa chachu ya kudumisha amani nchini.
ambapo
alisema TAKUKURU imekuwa chachu ya kuwafanya wafanyakazi wa mahakama kuogopa
kuomba na kupokea Rushwa na kusababisha kufanya kazi kwa maadili
Kyaruzi alisema taasisi hiyo ni mdau mkubwa wa
Mahakama kwa kuwa nayo inafanya kazi kwa lengo la kuwatumikia wananchi hivyo
kama itajikita kwa watumishi wa kada zote za mahakama itasaidia kupunguza
Rushwa kwa wananchi pamoja na watumishi hao
Alisema taasisi hiyo kama itajikita kwa watumishi hao
ana imani itatendeka zaidi na kuongeza kasi ya utendaji kazi ingawa kwa mwaka
jana mahakama zote za mwanzo pamoja na ya wilaya zimefanya vizuri kwa kumaliza
kesi zote kasoro mahakama mbili tu ambazo nazo ziko katika hatua ya
mwisho kumaliza
Pia kyaruzi alisema katika kipidi cha mwaka jana
jumla ya kesi 1118 zilifunguliwa lakini 1105 zimekwisha na bado kesi 13 hali
ambayo ni hatua nzuri ya utekelezaji wa agizo la jaji mkuu la kutaka mahakama
zote nchini kuanza na kesi sufuri kila mwaka unapoanza
Kwa upande wake mwakilishi wa mkuu wa TAKUKURU mkoa
wa Takukuru wa Kahama Amos Lugomela alisema Taasisi yake haipendi kuona
watumishi wanakamatwa kwa kuomba na kupokea rushwa isipokuwa inapenda kuona
watumishi wanafanya kazi kwa maadili ya kazi yao bila kuomba Rushwa
Lugomela aliwataka watumishi hao wote kutoka mahakama
za Mwanzo na ile ya wilaya kuwatumikia wananchi bila upendeleo wowote kwani
kuomba na kupokea Rushwa kwa wananchi masikini wanaohitaji huduma ni dhuluma
ambayo haikubaliki kwenye jamii na kwenye maadili ya utendaji kazi za umma
Naye mkuu wa wilaya ya Kahama Vita Kawawa aliwaomba
viongozi wa Mahakama Kutenga siku ya kutoe elimu ya Kisheria kwa wananchi wa
vijijini ambao wengi wao wamekuwa wakipoteza haki zao kwa kutojua sheria na
ndio nafasi inayotumiwa na watu wasiokuwa waaminifu kuwadhulumu mali zao
Kawawa alisema hali ya kutojua sheria kwa wananchi wa
vijijini hata watumishi wa Mahakama wasiokuwa waaminifu wamekuwa wakiitumia
kupinda haki kwa maslahi yao hali ambayo kama mahakama zitatoa Elimu kwa
wananchi dhuluma za kudhulumiwa haki zao hasa wanawake zitapungua
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI