Monday, February 8, 2016

MAKAMISHINA ZEC WAMPINGA JECHA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



HALI ya Kisiasa Zanzibar inazidi kuwa tete,baada ya baadhi ya Makamishina wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar “ZEC”,kujitokeza hadharani na kupinga marudio ya uchaguzi uliotangazwa na Mwenyekiti wa Tume
hiyo,Jecha Salum Jecha kuwa utafanyika uchaguzi wa marudio,kuwa si halali kwakuwa ni maamuzi yake binafsi.

Tamko hilo lilitolewa na makamishina wawili wa ZEC,Nassoro Khamis Mohamed na Ayoub Hamad,jana Jijini Dar Es Salaam walipoongea na vyombo mbalimbali vya habari nchini,ambapo walidai  tukio la kufutwa kwa uchaguzi huo lilitanguliwa na matukio kadhaa ambayo yalionyesha wazi kuwa kuna kikundi cha watu ambacho kinamshauri mwenyekiti wa tume hiyo.

Makamishina hao wamejitokeza hadaharani kumpinga Jecha wakati wadau mbalimbali wa masuala ya kisiasa wakipinga kile kinachoendelea visiwani Zanzibar, kwa madai kuwa uchaguzi huo sio halali kulingana na matukio yaliyotokea tangu kufanyika kwa uchaguzi halali wa Oktoba 25 mwaka jana.

Wakizungumza na wanahabari Jijini Dar es salaam makamishna hao, walisema wanapinga kufanyika kwa uchaguzi huo wa marudio kutokana na kuvurugwa kwa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984,tangu tukio la kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa mwaka jana,kutokana na Mwenyekiti wa Tume hiyo kutokuwa na mamlaka ya kisheria kufuta uchaguzi huo pasipo kuwashirikisha makamishna wa tume hiyo.
Walisema   sababu nyingine inayowafanya kupinga uchaguzi wa marudio ni kutokana na kukamilika kwa uchaguzi wa mwaka jana ambapo uchaguzi huo ulikuwa umekamilika na baadhi ya washindi wa viti vya uwakilishi na udiwani walishakabidhiwa vyeti vyao na mawakala kusaini kuwa uchaguzi huo hauna kasoro hivyo wanashangaa kuambiwa kuwa uchaguzi huo ulikuwa na kasoro nyingi zilizopelekea kuubatilisha uchaguzi huo.
Waliongeza kurudiwa kwa uchaguzi huo ambao unatarajiwa kutumia zaidi ya bilioni saba hadi kukamilika kwake ni matumizi mabaya ya rasilimali za taifa kwani uchaguzi Zanzibar ulishafanyika na tayari na kinachoendelea ni mbinu za kuubatilisha uchaguzi huo.
Mmoja wa Makamishina hao Nassoro Khamis alikiri kuwa Tarehe 26 oktoba mwaka jana, CCM iliikabidhi  barua ya malalamiko na kumtaka mwenyekiti na tume kufuta uchaguzi huo wakati tayari vyeti vya ushindi,viliishatolewa kwa wahusika na Mwenyekiti aliitisha kikao cha tume na kilichoafikiana  kuwa maombi hayo hayakuwa na mashiko hivyo mchakato uendelee.
Khamis alidai baada ya maamuzi ya tume, siku iliyofuata Mwenyekiti Jecha hakutokea katika ujumuishaji wa matokeo kwa siku nzima na ndipo waliposikia kuwa ametangaza kufuta uchaguzi bila kuwashirikisha wajumbe wengine wa tume hiyo   ndipo ofisi  ilipozungukwa na wanajeshi na kuamuriwa kutofanya lolote huku Jaji Mkuu wa Mahakama ya Zanzibar  akikamatwa na kupekwa polisi.
Walisema kuwa kwa matukio kama hayo wanaamini kuwa tume hiyo imeacha kufanya kazi zake kisheria na sasa inafanya kazi kisiasa jambo ambalo linampotezea sifa Mwenyekiti wa ZEC kuendelea kuiongoza tume hiyo,huku wakitoa wito kwa wajumbe wengine ndani ya tume hiyo kuacha kufuata mkumbo na kuamua kusimamia sheria inavyosema ili kuwapatia Wazanzibar haki yao ya Kikatiba.


Bottom of Form








Bottom of Form

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI