![]() |
WAZIRI wa Habari,Utamaduni,Wasanii na Michezo,Nape Nnauye. |
BAADHI ya Wakazi wa Kahama,wamepinga
vikali kauli aliyotoa Waziri wa habari,
utamaduni, wasanii na michezo,Nape Nnauye, kutaka vikao vya bunge kufanyika bila ya
kurushwa moja kwa moja na luninga ya
shirika la utangazaji nchini (TBC);kwa madai ni kuiminya demokrasia na haki ya kufahamu kwa wakati kinachoendelea
Bungeni.
Mshauri wa masuala ya Biashara
wilayani Kahama,Moses Mwanakulya,alishangazwa na kauli hiyo ambayo
hakubaliani nayo kufuatia TBC kuwa chombo cha umma kinachoendeshwa kwa kodi za
Watanzania wa kipato cha chini hivyo haistahili kuchukua maamuzi hayo.
Mwanakulya alisema kwa kauli ya Nape
inadhihirisha kuwa serikali ina agenda ya siri,pia haitaki wananchi wake
wafahamu kinachoendelea kwa kuogopa wananchi wake kufahamu baadhi ya mambo
kutokana na kukabiliwa na changamoto nyingi hasa kwakuwa Rais magufuli aliingia
na matumaini makubwa.
“Kuna mambo amabyo serikali inaogopa
wananchi wake wasiyajue,lakini ni makosa makubwa kama TBC inasema inazidiwa
gharama basi iruhusu mashirika mengine yarushe,kwanini kuwe kuna kikwazo kwa
mashirika mengine ilhali Watanzania wanataka wafahamu wawakilishi wao wanasema
nini Bungeni?”Alihoji Mwanakulya.
Kwa upande wake mkazi wa Kata ya
Majengo,Hassani Kagoma,alisema Serikali ni budi itambue demokrasia ina nafasi
yake,hivyo kauli ya Nape ina minya demokrasia na kukiuka Katiba inayotoa nafasi
ya uhuru wa kupata habari,na kuiomba kuondokana na kuwa na maamuzi ya kutaka
kauli za viongozi zifuatwe pasipo kujali sauti za wananchi.
Aliomba mamlaka zinazomzidi maamuzi
Nape zitafakari na kuondoa hoja hoja hiyo ambayo kimsingi inawanyima haki
Watanzania,hasa kwakuwa Waziri huyo anaonesha madaraka kumlevya kiasi cha
kushindwa kutambua tuko katika zama za dunia kuwa kijiji mimoja hivyo wananchi
kuhitaji taarifa na maamuzi ya bunge kuyapata kwa wakati.
Nae Mratibu wa Baraza la Vijana la
CHADEMA Wilaya ya Kahama,Elevant Charles,alisema kitendo hicho ni kuwanyima
haki Watanzania na kudai kama hoja ni gharama,watambue hicho ni chombo cha umma
na hakiendeshwi kibiashara bali kwa kodi za Watanzania,hivyo kuomba serikali
ibatilishe maamuzi hayo.
Kwa upande wake Sheikh wa Mtaa wa
Kahama,Sheikh Ramadhani Damka,alisema kauli hiyo ikitekelezeka itasababisha
wananchi kuwa na mashaka na uadirifu wa serikali kwa kuwanyima haki kwa
kutopata baadhi ya vitu moja kwa moja na kuingiwa na hisia kuwa kuna
mambo ambayo wanayaficha.
Sheikh Damka alisema kipindi hiki ni
cha utandawazi uliosababisha dunia ipo katika kiganja hivyo kauli hiyo
ikitekelezeka itaminya demokrasia nchini,hivyo aliomba uwazi uendelee ili
wananchi wafahamu Mwakilishi wao anawawakilisha ipasavyo na wamudu kumkosoa
pindi wakimuona anakengeuka maadili ya Kitanzania na kutowajibika kwa kile
walichomtuma.
Kufuatia maamuzi hayo ya serikali
yalisababisha kuibuka kwa Vurugu kubwa,ndani ya ukumbi wa bunge na kusababisha
kundi la polisi wa kutuliza ghasia kuingia ndani ya ukumbi huo na kuwatoa
wabunge wa upinzani ambao walikuwa wanapinga.
![]() |
WABUNGE wa Upinzani wakitolewa nje na Polisi |
Pamoja na Bunge kuahirishwa hadi
kikao chake cha jioni,bado hakutokea utulivu mbaya baada ya mwenyekiti Chenge
kutangaza kuwa kamati ya uongozi ya bunge imesema ratiba ya kikao cha bunge
iendelee kama kawaida,kauli ambayo haikuafikiwa na Wabunge wa Upinzani kiasi
cha kuibuka upya tafrani kwa kipindi kirefu ndipo polisi walipoingia ukumbini
na kuwatoa nje wabunge wa upinzani.
Kama vile haitoshi hata waandishi wa habari nao walitolewa nje na mkuu wa kitengo cha habari elimu na mawasiliano kwa umma,Owen Mwandumbya, hatua ambayo ili walazimu wanahabari kushindwa kutekeleza majukumu yao.
Kama vile haitoshi hata waandishi wa habari nao walitolewa nje na mkuu wa kitengo cha habari elimu na mawasiliano kwa umma,Owen Mwandumbya, hatua ambayo ili walazimu wanahabari kushindwa kutekeleza majukumu yao.
Kitendo ambacho baadhi ya wabunge wenye
taaluma ya habari wamekilaani kwa madai ya kuzuia kutangaza bunge ni hatua ya
mwanzo ya kuua uhuru wa habari nchini na hivyo serikali inabidi kujitazama upya.