Wednesday, January 27, 2016

WAANDISHI WAASWA KUTOKURUPUKA KUANDIKA HABARI ZA WAWEKEZAJI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO





WAANDISHI wa Habari wameaswa kufuata taratibu zinazohusika kufika katika maeneo ya wawekezaji hususani migodi ya dhahabu,kujionea utendaji kazi na si
kukurupuka kuandika na kutangaza taarifa potofu juu ya Mwekezaji.

Kauli hiyo ilitolewa na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu,unaomilikiwa na Kampuni ya ACACIA;Graham Crew,wakati akiongea na Waandishi wa Habari tisa kutoka mikoa ya Mwanza na Shinyanga,waliofanya ziara kujionea utendaji kazi wa Mgodi.

Crew alisema,Waandishi wa Habari ni washirika muhimu katika kumuunganisha Mwekezaji na jamii na kusaidia kusukuma maendeleo ya Taifa pindi kalamu wanazotumia zikitumika kwa weledi na kuzingatia miiko na maadili ya Habari.

Alisikitika kuona baadhi ya waandishi kutofahamu mazingira ya uwajibikaji wa Mgodi,lakini wamekuwa mstari wa mbele kutoa taarifa katika vyombo vya habari potofu ambazo zimekuwa zikichochea kutokuwepo mahusiano mema na jamii inayomzunguka Mwekezaji huyo.

“Msikurupuke pindi mnapoletewa tuhuma dhidi yetu,fanyeni uchunguzi na uandishi huo utakujengeni na kuaminika katika jamii”,Alisema Crew.

Kwa upande wake Meneja Ufanisi wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu,Elias Kasitila,aliwasihi waandishi wa habari kusimamia ukweli na usahihi,ili kuijengea heshima taaluma huku akisisitiza taaluma ya habari itumike kutangaza shughuli za kijamii zilizofanywa na Mwekezaji huyo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI