HATIMAYE
kiu ya familia ya soka hapa nchini iliyotokana na ugawaji wa tuzo,imetulia
baada ya Mtanzania;Mbwana Ally Samatta,kuwa mwanasoka bora
Afrika,kwa wachezaji
wanaocheza ndani ya bara hili.
Katika
utoaji huo wa Tuzo hizo za soka zilifanyika jana Jijini Lagos nchini Nigeria na
kuhudhuriwa na watu mbalimbali maarufu katika soka,barani Afrika.
Samatta
aliibuka mwanasoka bora kwa kuwashinda Muteba Kadiaba,ambaye ni kipa mkongwe wa
TP Mazembe na Bounedjah Baghdad wa Algeria anayekipiga Etoile du Sahel.
Aidha
Pierre Aubameyang alifanikiwa kubeba tuzo ya mwanasoka bora Afrika kwa mwaka
2015 na kumpiga kumbo Yaya Toure, aliyewahi kubeba tuzo hiyo mara tatu
mfululizo katika kipengele cha tuzo linalohusisha
wanasoka wanaocheza nje ya bara la Afrika.
Aubameyang
ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Gabon anakipiga katika kikosi cha
Borussia Dortmund.
Yaya
anayekipiga anayekipiga katika kikosi cha Man City alishika nafasi hiyo huku nafasi
ya pili ikienda kwa Andre Ayew ambaye aliongozana na baba yake, Abeid Pele.
Kwa upande wa mwamuzi bora wa soka mwaka 2015,tuzo ilienda
kwa Bakary Papa Gassana wa Gambia,kwa kuwashinda waamuzi wengine mahiri wawili;Alioum
wa Cameroon na Ghead Grisha- kutoka Misri.
Watanzania
wengi walikuwa wakisubiri kwa hamu kufanyika kwa tuzo hizo ili Samatta aweke
rekodi barani Afrika na kutimiza miongoni mwa ndoto alizonazo mwanasoka huyo.