![]() |
MCHUNGAJI Christopher Mtikila enzi za uhai wake. |
HABARI mpasuko zilizotufikia
hivi punde,zinaeleza Mwenyekiti wa Chama cha DP nchini Tanzania, mchungaji
Christopher Mtikila amefariki dunia,kutokana na
ajali ya gari.
ajali ya gari.
![]() |
GARI alilokuwemo Mchangaji Mtikila. |
Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Jafar Ibrahim amethibitisha
kutokea kwa tukio hilo na kwamba watu wengine watatu waliokuwa katika gari hilo
wamekimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu.
"Kwa maelezo ya dereva,gari ndogo aina ya Salon waliyokuwa wanasafiria iliacha njia wakiwa wanaelekea jijini Dar es salaam,ikapinduka,ilikuwa na watu wanne akiwemo dereva na mchungaji Mtikila,hawa watatu ni majeruhi na mchungaji Mtikila inasemekana amefariki,mwili wa marehemu na majeruhi wako njia wakielekea hospitali ya Tumbi",amesema Kamanda Ibrahim.
Amesema bado wanachunguza chanzo cha ajali hiyo...
Mtikila alitangaza kugombea Urais kupitia chama chake cha DP lakini chama chake ni moja ya vyama ambavyo vilikatwa kutokana na kutotimiza vigezo vilivyokuwa vinatakiwa.
"Kwa maelezo ya dereva,gari ndogo aina ya Salon waliyokuwa wanasafiria iliacha njia wakiwa wanaelekea jijini Dar es salaam,ikapinduka,ilikuwa na watu wanne akiwemo dereva na mchungaji Mtikila,hawa watatu ni majeruhi na mchungaji Mtikila inasemekana amefariki,mwili wa marehemu na majeruhi wako njia wakielekea hospitali ya Tumbi",amesema Kamanda Ibrahim.
Amesema bado wanachunguza chanzo cha ajali hiyo...
Mtikila alitangaza kugombea Urais kupitia chama chake cha DP lakini chama chake ni moja ya vyama ambavyo vilikatwa kutokana na kutotimiza vigezo vilivyokuwa vinatakiwa.