Tuesday, August 11, 2015

WANAWAKE WAONYWA KUTOTUMIKA KUPATA VIONGOZI WABOVU.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

MWEZESHAJI katika semina hiyo,Franuel Reuben.


inaweza kusababisha kuchagua viongozi wasio na sifa, sambamba na uchungu wa kutetea rasilimali za Taifa.



BAADHI ya washiriki katika semina hiyo.


Mzuka alisema wanawake wamekuwa wakirubuniwa kwa kupewa rushwa hali ambayo wamekuwa wakitumika kama daraja la kujipatia madaraka katika chaguzi mbalimbali huku wakishindwa kujitokeza kuwania nafasi za uwakilishi kwa kuhofia kuombwa rushwa ya ngono.

“Wanawake wanashindwa kujitokeza kuwania nafasi za uwakilishi kutokana na kutokuwa na pesa za kuhonga kwa viongozi wa vyama vya siasa ili viwapitishe,na kibaya zaidi pia hutumika kuhongwa khanga,sukari na chumvi ili kupitisha viongozi wabovu katika chaguzi ambao utumishi wao hujali maslahi yao kuliko ya umma,”Alisema Mzuka.

MKUU wa Takukuru wilayani Kahama,Enock Ngailo.


Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa wilayani Kahama,Enock Ngailo,alisema wanawake wanapaswa kutopokea rushwa kutoka kwa wagombea,vinginevyo watakuwa wanajinyima haki zao za msingi za kuchagua kiongozi mwenye  maslahi na umma.

Aliongeza kuwa ili mwanamke aweze kupata maendeleo kwenye jamii ni lazima achague kiongozi mtetezi wa maslahi ya umma,ambaye hakupatikana kwa njia ya Rushwa,na mwenye uwezo wa kukemea suala hilo kwenye jamii inayosababisha watu wengi kukosa haki zao.

MSHIRIKI katika semina hiyo,Paul Ntelya,akichangia mada.


Nae mwakilishi wa mkuu wa Polisi wilaya ya Kahama,Dismas Kifunde,aliwataka wanawake kutoa taarifa kwenye vyombo vya usalama pindi wanapoona viashiria vya uvunjifu wa amani,ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua kali za Kisheria.

SHDEPHA+ inatekeleza mradi huo,unaoratibiwa na OXFAM Ireland na kufadhiliwa na UKAIDS kutoka Uingereza na USAIDS ya Marekani,ikiwa na lengo la kujadili na kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazowakabili wanawake katika harakati za kuwania uwakilishi na upigaji kura.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI